Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Uchaguzi Ujerumani: Ushindi usio wa kishindo kwa Merkel

MTEULE THE BEST

Angela Merkel mjini BerlinHaki miliki ya pichaAFP
Image captionJukumu la Bi Merkel la kuunda serikali ya muungano huenda likachukua miezi
Angela Merkel anaonekana amechoka, alipowasili katika makao makuu ya chama chake baada ya kumalizika uchaguzi.
Akitoka katika gari lake alitabasamu kwanza kwa wapiga picha waliomsubiri alafu kwa wafuasi wa chama chake waliokusanyika katika makao ya chama cha CDU.
Kansela alitambua kwamba huenda angeshinda uchaguzi huu. Lakini sio ushindi alioutarajia yeye binfasi wala chama chake. Ni matokeo mabaya kwa chama hicho cha kihafidhina chini ya utawala wake.
Huenda ni matokeo ya uamuzi wake kuwafungulia mlango mamilioni ya wakimbizi kuingia Ujerumani.
Akihotubia wafuasi wa chama chake, Bi Merkel amekiri kwamba miaka minne iliyopita imekuwa migumu. Licha ya hayo chama chake kimefanikiwa kwa lengo lake - Kuibuka mshindi.
Nderemo hazikuwa kubwa kwasababau ushindi mkuu wa uchaguzi huu ni wa AfD.
Upande wa pili wa mji huo, katika chumba kilicho sheheni vibofu vya rangi ya samawati na nyeupe, wafuasi wa chama kinachopinga uhamiaji, kinachopinga Umoja wa Ulaya walisherehekea ilipobainika
kwamba hawatoingia bunge kwa mara ya kwanza tu, lakini kwamba watakuwa wafuasi wa chama cha tatu kwa ukubwa bungeni baada ya chama cha Merkel CDU na wapinzani wake wa karibu Social democratic - SPD.
Waandamanji wanaopinga chama cha mrengo wa kulia AfDHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionWaandamanaji wanaopinga chama cha mrengo wa kulia AfD
Lakini kampeni ya ubaguzi ya AfD na ghasia zilizo tatiza mikutano ya Merkel huenda ni mfano wa yanatorajiwa. Nje ya makao ya chama hicho, maafisa wa polisi wana watazama kwa makini waandamanaji
wanaokipinga AfD dhidi ya kile wengi wanaona ni maendeleo ya kushtusha ya kisiasa.
Kuna migawanyiko, na hisia ya kutoridhia katika taifa hili. Baadhi wanatishiwa na wanachokitaja kuwa ni kukuwa kwa siasa za utaifa za mrengo wa kulia.
Bi Merkel sasa ni lazima atafuta washirika wa kuunda serikali ya muungano. Na ni lazima aishawishi nchi yake na pengine baadhi ndani ya chama chake, kwamba anastahili kazi hiyo.
Zimekuwa ni kampeni ndefu na za kutia uchungu. Huenda Merkel ameshinda lakini ushindi wake hauna kishindo
Uchaguzi huu utaingia katika vitabu vya historia kwa sababu mbili. Huenda Angela Merkel ameshinda hatamu ya nne uongozini lakini ni matokeo mabaya kuwahi kushuhudiwa kwa chama chake.
Na pili wanasiasa wa mrengo wa kulia wanaoshinikiza utaifa, sasa wamejiunga katika utawala wa Ujerumani.
Kilicho kawaida ya siasa katika nchi nyingine nyingi Ulaya kilichodhaniwa hakiwezi kufanyika katika Ujerumani ya baada ya vita vikuu. Sasa kimekuwa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...