Haki miliki ya pichaEPAImage captionMpalestina awapiga risasi na kuwaua raia watatu wa Israel
Watu watatu raia wa Israel wameuawa kwa kupigwa risasi na raia wa Palestimna katika mlango wa kuingia kwenye makao ya walowezi wa kiyahudi eneo la Har Adara lililo ukingo wa magharibi.
Mtu mwenye bunduki wa umri wa miaka 37 kutoka kijiji kilicho karibu pia alipigwa risasi na kufariki baadaye.
Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema mauaji hayo yamesababishwa na uchochezi upande wa palestina.
Mauaji hayo yanafanyika wakati mjumbe wa Rais Donald Trump eneo la Mashariki ya Kati Jason Greenblat, anapowasili Jerusalem kufufua mazungumzo kati ya Israeli na Palestina.
Image captionZaidi ya wayahudi 600,000 wanaishi karibu makao 140 yaliyojengwa tangu mwaka 1967
Ikulu ya Marekani inasema kuwa imejaribu kufanya mikakati wa kuyafufua mazungumzo tangu Donald Trump aingie madarakani mwezi Januari lakini hakujakuwa na dalili za kuwepo hatua.
Mazungumzo ya amani kati ya pade hizo mbili yalivunjika mwezi Aprili mwaka 2014.
Polisi wanasema kuwa mtu huyo mwenye silaha anayetajwa na vyombo vya habari nchini Israeli kama Nimer Jamal, alishambulia baada ya kugundua kuwa alishukiwa na walinzi karibu na mlango wa eneo la Har Adar.
Aliwapiga risasi walinzi wawili na polisi wa mpaka kwa karibu, na kumjeruhi vibaya mtu mwingine kabla ya kupigwa risasi na vikosi vya usalama.
Haki miliki ya pichaEPAImage captionAliwapiga risasi walinzi wawili na polisi wa mpaka kwa karibu, na kumjeruhi vibaya mtu mwingine
Alitoka kijiji cha Beit Surik, karibu maili moja mashariki mwa Har Adar.
Eneo hilo liko karibu kilomita 18 kaskazini magharibi mwa Jurusalem.
Karibu Wapalestina 36,000 wana vibali vya kufanya kazi katika makao ya wayahudi ambapo ulinzi wa kuyalinda dhdi ya mashambulizi ni mkali.
Zaidi ya wayahudi 600,000 wanaishi karibu makao 140 yaliyojengwa tangu mwaka 1967, kwenye ukingo wa magharibi na Mashariki mwa Jerusalem.
Haki miliki ya pichaISRAELI POLICEImage captionPolisi walitoa picha ya bunduki aliyoitumia
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni