Kiongozi wa China akutana na mwenzake wa Korea Kaskazini
Kitengo cha taifa cha habari nchini Korea Kaskazini kimeripoti kwamba mjumbe maalum wa China Song Tao amefanya mazungumzo na Choe Ryong-Hae , ambaye ni mshauri wa karibu wa rais wa Korea Kaskazini Kim Jong un .
Ziara hiyo ambayo ni ya kwanza kuwahi kufanywa na afisa mwanadimizi wa China katika kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja inajiri wakati ambapo kuna hali ya wasiwasi mwingi kati ya washirika hao wawili na inafuatia ziara ya rais Trump katika eneo hilo.
Trump amekuwa akiishinikiza China kuiwekea vikwazo vya Umoja wa mataifa Korea Kaskazini
China haijatoa maelezo ya ziara hiyo, lakini vyombo vya habari vya Korea Kaskazini vimesema kwamba bwana Song alisisitiza kuhusu mpango wa Bejing wa kuimarisha urafiki wa miaka mingi uliokuwepo kati ya mataifa hayo mawili.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni