Mwanamfalme wa Saudia amemtaja kiongozi wa kidini wa Iran kuwa 'Hitler' mpya wa eneo la mashariki ya kati huku kukiwa na wasiwasi kati ya mataifa hayo mawili
Mwanamfalme MOhammed bin Salman wa Saudia na rais Hassan Rouhani wa Iran
Mwanamfalme wa Saudia amemtaja kiongozi wa kidini wa Iran kuwa 'Hitler' mpya wa eneo la mashariki ya kati huku kukiwa na wasiwasi kati ya mataifa hayo mawili.
Akitaja kuongezeka kwa ubabe wa Iran katika eneo hilo, Mohammed Bin Salman amesema kuwa ni vyema kuzuia yaliotokea barani Ulaya katika eneo la mashariki ya kati.
Saudia na Iran ni wapinzani na wamekuwa wakishutumiana kwa kuchochea ukosefu wa uthabiti katika eneo la mashariki ya kati.
Hatahivyo hakuna tamko lolote liliotolewa na Iran kufuatia matamshi hayo ya hivi karibuni.
Akizungumza na gazeti la The New York Times , Mohammed bin Salman alisema kuwa Iran haiwezi kuruhusiwa kusambaza ushawishi wake.
''Tulijifunza kutoka Ulaya kwamba kujionyesha kwamba wewe ni mtu mzuri hakufanikiwi''.
''Hatutaki Hitler mpya wa Iran kurudia yaliotokea barani Ulaya katika eneo la mashariki ya kati'', alisema akimtaja kiongozi wa kidini wa Iran Ayatollah Ali Khamenei.
Mohammed bin Salman, ambaye ndio mtawala mkuu wa ufalme huo amekuwa na msimamo mkali dhidi ya Iran tangu alipochukua mamlaka katika kipindi cha miaka miwili iliopita.
Mapema mwezi huu ,aliishutumu Iran kwa kile alichosema ni uchokozi wa kivita akiilaumu kwa shambuio la kombora lililolenga mji mkuu wa Saudia, Riyadh, na waasi katika taifa jirani la Yemen.
Iran imekana kwamba ilihusika.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni