Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TETESI ZA SOKA LEO

MTEULE THE BEST


Mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola analenga kumnunua Riyad Mahrez katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari (Don Balon via The Sun)


Riyad Mahrez






Nahodha wa zamani wa klabu ya West Brom Derek McInnes, anayeisimamia Aberdeen, ni miongoni mwa wagombea wa kuchukua mahala pake mkufunzi wa klabu hiyo aliyefutwa kazi Tony Pulis kama mkufunzi. (The Scottish Sun)

Hatahivyo mashabiki wa West Brom wanamtaka mkufunzi wa zamani wa Everton kuchukua mahala pake Pulis. (Express & Star)

Mkufunzi wa zamani wa klabu ya West Ham Alan Pardew, meneja wa zamani Nigel Pearson na mkufunzi wa timu ya Ireland Martin O'Neill ni miongoni mwa wakufunzi walioorodheshwa katika kuchukua kazi ya meneja wa West Brom job. (Guardian)

Sam Allardyce

Mkufunzi wa zamani wa Uingereza Sam Allardyce pia analengwa kuichukua kazi ya ukufunzi wa klabu ya West Brom na imebainika kwamba baadhi ya wachezaji wa klabu hiyo walikuwa wakitaka mkufunzi Pulis kuondoka. (Mirror)

Pulis ni miongoni mwa wakufunzi wanaopigiwa upatu kumrithi Paul Clement iwapo Swansea itamfuta kazi na pia atakuwa miongoni mwa wale wanaopigania kazi ya kuifunza Wales. (Daily Telegraph)

Mchezaji wa zamani wa Liverpool Dirk Kuyt anaamini mchezaji wa Uholanzi Virgil van Dijk ni mchezaji mzuri anayefaa kujiunga na klabu hiyo ya Anfield. (Sky Sports via Express)

Phillipe Countinho

Philippe Coutinho alimpiku Robbie Fowler na Michael Owen baada ya kutoa usaidizi wa goli la 31 la Liverpool siku ya Jumamosi.

Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Manchester United Andy Cole amietaka klabu yake ya zamani kumzuia mshambuliaji wa Ufaransa Anthony Martial, huku akidai kwamba Marcus Rashford ana uwezo mkubwa wa kuimarika zaidi. (ESPN)

Jose Mourinho

Kwengineko mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho amepigwa jeki kufuatia habari kwamba Bayern Munich wamejiondoa katika kumwania mshambuliaji wa Atletico Madrid Antoine Griezmann, 26. (Daily Star)

Mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola analenga kumnunua Riyad Mahrez katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari (Don Balon via The Sun)

Mesut Ozil

Kiungo wa kati wa Arsenal na Ujerumani Mesut Ozil, 29, anasakwa na klabu ya Schalke, klabu ambayo alianza kushiriki soka ya kulipwa .(Kicker - in German)

Mshambuliaji wa Watford na raia wa Brazil Richarlison, 20, anasakwa na baadhi ya vilabu nchini China baada ya kufunga mabao 12 katika mechi 12 za ligi ya Uingereza. (Watford Observer)

Daniel Sturridge, 28,

Mkufunzi wa Liverpool Jurgen Klopp amekataa kumuuza Daniel Sturridge, 28, katika soko la uhamisho la mwezi Januari. (Liverpool Echo)

Kipa wa Liverpool na Wales Danny Ward, 24, na mshambuliaji Ben Woodburn, 18, wanatakiwa na mkufunzi mpya wa Sunderland Chris Coleman. (Sunderland Echo)

Celtic huenda ikamuania beki wa klabu ya Reading mwenye umri wa miaka 24-Liam Moore mnamo mwezi January. (Reading Chronicle)


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...