Ruka hadi kwenye maudhui makuu

RUSSIA NA CHINA ZAFANYA DORIA YA PAMOJA MAREKANI YALIA

Doria ya pamoja ya Urusi - China yazua tumbo joto Japan na Korea Kusini




Korea Kusini ilisema kuwa ndege ya kijeshi ya Urusi aina ya A-50 ilikiuka anga yake mara mbili

Urusi inasema kuwa imetekeleza doria yake ya kwanza ya pamoja na China , hatua iliyozifanya Korea Kusini na Japan kutuma ndege za kivita angani.


Waziri wa ulinzi nchini Urusi amesema kuwa ndege nne aina ya bombers zikisaidiana na zile za kivita zilipiga doria katika njia ambayo hazikupangiwa kupitia katika maji ya Japan na bahari iliopo mashariki mwa China.

Korea Kusini inasema kuwa ndege zake zilirusha makombora ya kutoa onyo wakati ndege za kijeshi za Urusi zilipoingia katika anga yake. Japan imelalamika kwa Urusi na Korea Kusini kwa tukio hilo.



Kisa hicho kilitokea juu ya visiwa vinavyozozaniwa vya Dokdo/Takeshima ambavyo vinamilikiwa na Korea Kusini lakini Japan pia inadai kuwa vyake.

Korea Kusini inasema kuwa ndege za kijeshi za Urusi na China ziliingia katika anga yake ilio na ulinzi mkali ya KADIZ siku ya Jumanne alfajiri na kwamba ndege moja ya kijeshi ya Urusi aina ya A-50 ilikiuka sheria za kimataifa na kuingia katika anga yake mara mbili karibu na visiwa hivyo. Urusi imekana madai hayo.

Ndege za kijeshi za Urusi na China aina ya Bombers mara kwa mara zimekuwa zikipitia eneo hilo katika miaka ya hivi karibuni lakini hicho ndio kisa cha kwanza kutokea kati ya Urusi na Korea Kusini.

Je Moscow inasemaje?

Wizara ya ulinzi inasema kuwa ndege zake mbili za kijeshi aina ya Tu-95MS zinazobeba makombora zilishirikiana na ndege nyengine mbili za China aina ya Hong-6k katika doria ambayo ilipitia katika njia ambayo hazikupangiwa juu ya anga ya maji yasiomilikiwa na taifa lolote.

Ndege hizo zilisaidiwa na ndege za kijeshi aina ya A-50 pamoja na Kongjing-2000 zinazotumika kutoa onyo .

Luteni jenerali Sergei Kobylash alisema kwamba wakati wa doria hiyo walifukuzwa mara 11 na ndege za kigeni.

Aliwashutumu manohodha wa ndege za Korea kusini kwa kufanya 'hatari' na kundi hilo la angani pamoja na hatari ya usalama wa ndege hizo.

Anasema kwamba ndege hizo za Korea Kusini zilirusha alama za moshi kutoa onyo.

Doria hiyo alisema ilifanyika zaidi ya kilomita 25 mbali na visiwa vya Doldo/Takeshima , na akawashutumu manahodha wa Korea kwa kufanya uhalifu angani.

Alisema kwamba Urusi ililalamika kwa Korea Kusini kuhusu vitendo vya hatari vya manahodha wake.

Muungano utakaoipatia Marekani tumbo Joto

Kulingana na mchanganuzi wa BBC wa maswala ya Ulinzi Johnathan Marcus , doria ya kwanza ya pamoja angani ilioshirikisha Urusi na China katika eneo la pacific Asia , inatuma ishara kuhusu hatua zilizopigwa na Mscow na Beijing.

Ijapokuwa nchi hizo mbili hazijaanzisha muungano rasmi wa pamoja zoezi hilo la pamoja ni kubwa na la kisasa.

Hatua hii ni ishara ya wazi ya uhusiano mzuri wa kiuchumi na kidiplomasia kati ya mataifa mawili ambayo licha ya kwamba bado yana wasiwasi yanaendelea kuleta uhusiano wa pamoja,



Yote mawili yana maono yanayofanana kuhusu ulimwengu wa sasa yakiwa maadui ya demokrasia iliopo magharibi,

Yakiwa tayari kukuza mbadala wa kutetea uhuru wao mbali na kuwa tayari kuonyesha uwezo wao dhidi ya mataifa mengine.

Swala hili linatoa changamoto kubwa kwa mkakati wa Marekani.

Ndoto ya Washington ni kuimarisha uhusiano wake na Urusi inayodorora na China inayoendelea kuimarika na tayari kuipiku Marekani kama taifa lenye uwezo mkubwa kiteknolojia na kiuchumi katika kipindi cha miaka kadhaa ijayo.

Je Korea Kusini inasemaje?

Jeshi la Korea Kusini linasema kuwa ndege hiyo ilikuwa mojawapo ya ndege tatu za Urusi na mbili za jeshi la China ambazo ziliingia katika anga ya KADIZ , ambapo ndege za mataifa mengine ni sharti zijitambulishe.

Ndege za kijeshi za Urusi na China zimekuwa zikiingia katika eneo hilo katika miaka ya hivi karibuni.

Hatahivyo Korea Kusini inasema kuwa moja ya ndege hizo ilipaa zaidi na kuingia katika anga ya nchi hiyo mwendo wa saa tatu alfajiri saa ya Korea.


Ndege za Kijeshi za Korea Kusini F-15k na F-16k zilitumwa kwenda kuizuia.

Mkuu wa kitengo cha usalama nchini Korea Kusini Chung Eui-yong amewasilisha malalamishi kwa baraza la usalama la Urusi na kulitaka kuchukua hatua kali.

''Tunakichukulia kitendo hiki kama kisichokuwa cha kawaida , na iwapo kitarejelewa tutachukua hatua kali, afisi ya rais wa taifa hilo ilimnukuu bwana Chung akisema. Hakujakuwa na tamko lolote kutoka China


Ndege ya kijeshi ya Korea Kusini aina ya F-15 ilitumwa kuizuia ndege hiyo ya Urusi

Na Japan Je?

Serikali ya Tokyo imewasilisha malalamishi dhidi ya Urusi na Korea Kusini.

Kwa kuwa inadaia umiliki wa visiwa hivyo, serikali ya Japan inasema kuwa Urusi ilikiuka anga yake.

Pia inasema kwamba jibu la Korea Kusini lilikuwa la kujutia.

Mkuu wa baraza la mawaziri nchini Japan Yoshihide Suga: Msimamo wa Japan kuhusu uumiliki wake wa Takeshima , hatua ya ndege za kijeshi za Korea Kusini kurusha moshi wa kutoa onyo ni swala ambalo haliwezi kukubalika na la kujutia.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...