Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Jeshi la Sudan kusini na tuhuma nzito

MTEULE THE BEST


Shirika la Amnesty International limevituhumu vikosi vya serikali ya Sudan Kusini vimeua, kubaka na kuwateka raia.
Shirika hilo la kimataifa la kutetea haki za binadamu limesema vitendo hivyo ni ukiukwaji wa makubaliano ya amani.
Ripoti hiyo, imetaja muda wa matukio hayo kuwa ni kati ya mwezi Agosti mwaka 2015 na Disemba 2015, kipindi ambacho vijiji pia vilichomwa moto.
Zaidi ya watu milioni mbili wamekimbia makazi yao nchini Sudan Kusini tangu kuanza kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe miaka miwili iliyopita.
Ripoti hiyo inagusia ukiukwaji ambao umeathiri mtu mmoja mmoja na vijiji katika nchi ya Sudan Kusini.
Amnesty inasema imefanya mahojiano na watu walioshuhudia wanaume kwa wanawake wakipigwa risasi na makundi yaliyokuwa yakishambulia.
Baadhi ya watoto na wazee wanaripotiwa kuchomwa moto wakiwa hai huku watoto wa kike wakibakwa mfululizo.
Mashuhuda wanasema, wanajeshi walivalia sare za jeshi pindi walipovamia.
Katika siku zilizopita, Umoja wa Mataifa pia umewahi kulishutumu jeshi la Sudan Kusini na makundi yanayoshirikiana nayo kwa vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu.
Hata hivyo, serikali ya Sudan Kusini imekana vikosi vyake kuhusika na tuhuma hizo.
Ingawa chama tawala na waliokuwa waasi wamesaini makubaliano ya amani na kuunda serikali ya pamoja, lakini bado kuna hali ya wasiwasi baina yao.
Hali hii imeonekana hivi karibuni katika mauji yaliyofanyika mjini Juba.
Riek Machar ambae yuko upinzani nafasi yake ya ukamu wa rais imechukuliwa na aliyekuwa mshirika wake wa karibu Taban Deng Gai.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...