Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Wakenya warefu zaidi kwa kimo Afrika Mashariki

MTEULE THE BEST

Dunia

Wanaume wa wanawake kutoka Kenya ndio warefu zaidi eneo la Afrika Mashariki kwa wastani kwa mujibu wa utafiti ambao matokeo yake yametolewa leo.
Utafiti huo, ambao matokeo yake yamechapishwa katika jarida la eLife yanaonesha kimo cha wastani miongoni mwa wanaume wa Kenya ni sentimeta 169.64 na wanaume sentimeta 158.16.
Utafiti huo ndio wa kina zaidi kufanywa, kwa mujibu wa watafiti hao, na uliangazia matokeo kutoka utafiti 1,472 uliofanywa katika mataifa 200.
Ulifuatilia kimo cha watu waliozaliwa mwaka 1896 hadi wale waliozaliwa mwaka 1996 ambao walitimiza umri wa miaka 18 mwaka 1914 hadi mwaka 2014. Waliochunguza kote duniani ni watu 18.6 milioni.
Kimo cha watu hutegemea lishe anayopata mama akiwa mjamzito pamoja na lishe ya mtoto anapokuwa mchanga.
Kimo cha mtu huhusishwa sana na afya ya mtu kwa jumla pamoja na hali ya maisha.

Watu warefu kwa kawaida huishi maisha marefu na huwa hawana matatizo mengi ya moyo na kupumua.
WanawakeImage copyrightGETTY
Image captionWanawake wa Guatemala ndio wafupi zaidi duniani
Utafiti huo wa kimo unaonesha Waafrika waliongeza urefu hadi kufikia miaka ya 1960 na 1970 lakini baada ya hapo wakaanza kupunguza kimo.
Watafiti waliohusika, miongoni mwao James Bentham na Majid Ezzati wa Chuo cha Imperial cha London, Uingereza, wanasema huenda hili limetokana na kusambaratika kwa mifumo ya afya, ongezeko la idadi ya watu na kubadilika kwa lishe hasa kutokana na watu wengi kuhamia mijini.
Ikizingatiwa kwamba ni kipimo cha wastani, kuwepo kwa watu wachache warefu sana katika baadhi ya nchi huenda kiliathiriwa na kuwepo kwa idadi kubwa ya watu wafupi.

Kimo cha wastani katika mataifa ya Afrika Mashariki na mataifa mengine ya karibu, kwa mujibu wa utafiti huo, ni kama ifuatavyo:

Wanaume (kimo cha wastani kwa sentimita)Wanawake (kimo cha wastani kwa sentimita)
Kenya169.64158.16
Burundi166.64154.02
Uganda165.62156.72
Tanzania164.80155.86
Rwanda162.68154.79
Zimbabwe168.57158.22
Sudan166.63156.04
Ethiopia166.23155.71
DR Congo166.80155.25
Congo Brazaville167.45157.57
Zambia166.52155.82
Malawi162.23154.40
Msumbiji164.80153.96

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...