Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Treni ya mwendo wa kasi yazinduliwa Nigeria

MTEULE THE BEST

Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria leo ameanzisha rasmi usafiri wa treni za kisasa zilizo na uwezo wa kuendeshwa kwa mwendo wa kasi.
Mradi huo wa kwanza kwa Nigeria umeigharimu nchi hiyo dolla million $850 .Reli hizo za kisasa kwa mfumo uitwao standard gauge(SGR) zilijengwa na kampuni kutoka Uchina.
Reli hizo ambazo ni mbili kwa moja yaani moja ni ya kwenda na nyengiine ya kurudi, zinaunganisha miji ya Abuja na Kaduna ambapo treni zitaweza kusafiri kwa mwendo wa kasi ya kilomita 120 hadi 150 kwa saa.
Wakati wa ufunguzi wa leo rais Buhari mwenyewe amesafiri kwa treni hiyo hivyo kuuanzishwa mfumo huo wa usafiri wa reli kwa umma.
Nauli kutoka mji huo mkuu wa Nigeria Abuja hadi mji wa Kaduna ulioko jimbo la kazkazini mwa nchi hiyo ni dolla $1:50 pekee.
Awali mradi huo ulikumbwa na chelewa chelewa za kisiasa baada ya kunzia utawala wa Obasanjo, ukapitia utawala wa Yardua hadi utawala wa Goodluck Jonathan na ndio sasa umekamilika tayari kwa matumizi katika utawala wa rais Buhari.
Image captionAbiria wakishuka katika treni mpya iliozinduliwa Nigeria
Zaidi ya hayo japo ujenzi wa reli ulikamilika Disemba 2014 huku treni zenyewe zikiwasilishwa nchini Nigeria miezi 15 baadaye.
Licha ya kuwa na utajiri mkubwa wa mafuta Nigeria imekuwa bila mfumo wa usafiri wa reli unaofanya kazi vyema kwa miongo kadhaa sasa kwa sababu ya ufisadi wa hali ya juu uliokuwa ukiendelea wakati wa tawala zilizopita.
Usafiri unaotumika sana ni ule wa barabara , ambao umekumbwa na changamoto nyingi kutokana na ajali nyingi zinazotokea, na pia magari na vilevile barabara uharibika sana kutokana na uzito wa magari ya mizigo yanayosafiri kwa mwendo mrefu.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...