Mourinho kuamua nafasi ya Rooney Uingereza

MTEULE THE BEST


Mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho ataamua ni safu gani ambayo Wayne Rooney atalichezea taifa lake ,kulingana na mkufunzi mpya wa Uingereza Sam Allardyce.
Rooney mwenye umri wa miaka 30 alicheza safu ya mashambulizi chini ya mkufunzi Roy Hodgson katika michuano ya Euro 2016.
Image copyrightPA
Image captionMkufunzi mpya wa Uingereza Sam Allardyce
Lakini Allardyce amesema kuwa ni mapema mno kuthibitisha iwapo Rooney,ambaye analiongoza taifa lake katika ufungaji wa mabao atasalia kuwa nahoda wa timu hiyo.
''Nadhani Wayne Rooney bado ana fursa kubwa kuchezea Uingereza'', alisema mkufunzi huyo mwenye umri wa miaka 61.
Image copyrightGETTY
Image captionMkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho
''Iwapo Jose atasema kwamba hatamchezesha katika safu ya kati na anamchezesha katika eneo la mashambulizi katika klabu ya Manchester United,itakuwa haina maana yoyote mimi kumchezsha katika safu ya kati''.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

ZIJUWE SHERIA 17 ZA SOKA

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

KUMTUMAINIA MUNGU