Ruka hadi kwenye maudhui makuu

''Lukaku aliondoka Everton kufuatia ujumbe wa uchawi''


Mabingwa wa ligi ya Uingereza Chelsea walikuwa wamewasilisha ombi la kutaka kumsajili Lukaku lakini badala yake akajiunga na Manchester United.


Mshambuliaji Romelu Lukaku aliamua kuondoka Everton baada ya ujumbe wa ''uchawi'' kumwambia ajiunge na Chelsea kulingana na mwenye hisa mkuu wa klabu ya Everton.


Mchezaji huyo wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 24 baadaye alijiunga na Manchester United kwa dau la pauni milioni 75 msimu wa uhamisho uliopita.


Farhad Moshiri aliwaambia wenye hisa katika mkutano na wachezaji kwamba mchezaji huyo alipokea ujumbe ''wa kwenda kuhiji Afrika'' wakati ambapo alitarajiwa kutia saini mkataba mpya katika klabu ya Everton.


''Alikuwa na uchawi na akapokea ujumbe aliotaka kwenda Chelsea'', alisema Moshiri.


Mabingwa wa ligi ya Uingereza Chelsea walikuwa wamewasilisha ombi la kutaka kumsajili Lukaku lakini badala yake akajiunga na Manchester United.


Mwezi Machi ajenti wa Lukaku Mino Raiola alikuwa amedai kwamba mkataba mpya wa kusalia Everton ulikuwa umekamilika asilimia 99.9.


''Tulimpatia kandarasi nzuri zaidi ya Chelsea na ajenti wake aliwasili kuja kutia kandarasi'' , Moshiri aliambia mkutano wa kila mwaka wa Everton.


Bilionea huyo wa Iran, Moshiri ambaye alikwa amewekeza dola milioni 150 katika deni la klabu hiyo, alisema kuwa Everton ilimpatia mshambuliaji huyo fedha nyingi ili kusalia.


''Swala la Lukaku halikuwa la kifedha. Iwapo nitaendelea kuwa miliki mkuu wa klabu hiyo maswala ya kifedha hayatakuwa tatizo''.Moshiri alisema kuwa Lukaku baadaye alimpigia simu mamake kabla ya mchezaji huyo kufichua kwamba alipokea ujumbe uliomwambia ajiunge na Chelsea


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...