Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za soka Ulaya Jumatano 10.01.2017

Alexis Sanchez


Manchester City wameipatia Arsenal dau la Ā£20m ili kumsajili Alexis Sanchez, 29, huku mshambuliaji huyo wa Chile akidaiwa kukubali malipo ya Ā£250,00 kwa wiki..(Guardian)


Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger anatarajiwa kuilipa Boca Juniors kitita cha pauni milioni 27 kumsajili Cristian Pavonkatikaligi Premia. (TyC Sports - in Spanish)


Wakati huohuo, Wenger anatarajiwa kukaa katika viti vya mashabiki katika uwanja wa Stamford Bridge kwa mechi ya Jumatano ya nusu fainali ya kombe la carabao baada ya kupigwas marufuku ya kukaa katika eneo la wakufunzi (Express)


Mkufunzi wa Real Madrid Zinedine Zidane anasema kuwa hataki kuwasajili wachezaji wapya katika dirisha la uhamisho licha ya kuwa nyuma ya viongozi wa ligi ya La Liga Barcelona.. (Reuters)


Mshambuliaji wa Manchester United Zlatan Ibrahimovic huenda akaondoka Old Trafford kabla ya kukamilika kwa msimu huu.


Raia huyo wa Sweden mwenye umri wa miaka 36 hana kandarasi na klabu hiyo. (Yahoo Sport)


Everton imetoa chanagamoto kwa Southampton katika ushindani wa kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Theo Walcott, 28, kwa Ā£20m. (Mail)


Liverpool na Arsenal watalazimika kulipa takriban Ā£90m kumsajiuli mshambuliaji wa Monaco Thomas Lemar, 22. (Mirror)


lakini kulingana na mwandishi wa Ufaransa Julien Laurens, huenda akachelewesha uhamisho wake Liverpool kutokana na michuano ya kombe la dunia (5 live's Euro Leagues podcast)


Winga wa Brazil Lucas Moura, 25, amekubali kujiunga na manchester United kutoka Paris St-Germain, ijapakuwa kitita cha uhamisho huo hakijakubalika kati ya vilabu hivyo viwili. (Gazetta dello Sport - in Italian)


Arsenal itawasilisha rasmi ombi jipya la kandarsi mpya ya kiungo wa kati wa Uingereza Jack Wilshere.


Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 anatarajiwa kuanza mazungumzo na Arsenal katika kipindi cha wiki moja ijayo na atalazimika kupunguza mshahara wake ili kusalia klabu hiyo. (Mirror


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...