Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za Soka Ulaya Jumatatu 08.01.2018

Antoine Griezman

Mshambuliaji wa Ufaransa Antoine Griezmann, 26, ataitisha pauni 400,000 kwa wiki kuzuia ofa ya Chelsea ili kujiunga na Manchester United. (Sun)

Chelsea wanamtaka mshambuliaji wa Borussia Monchengladbach na Ubelgiji Thorgan Hazard, 24, kujiunga na ndugu zake Eden, 27, na Kylian, 22, huko Stamford Bridge. (Bild - in German)

Liverpool wanamtaka mshambuliaji wa Monaco na Ufaransa Thomas Lemar, 22, kuchukua mahala pake Philippe Coutinho - na wanataka kufanya hilo wiki hii. (Mirror)

Manchester United na Chelsea zimemuulizia mshambuliaji wa Porto Mousa Marega, 26. (Metro)
VIDEO YA MAGOLI YA MANCHESTER UNITED


Thomas Lemar

Real Madrid walikuwa na nia ya kutoa ofa ya pauni milioni 177 kwa Coutinho kabla ya kukubali kujiunga na Barcelona kwa pauni milioni 142. (Mundo Deportivo - in Spanish)

Coutinho atafanyiwa uchunguzi wa kiafya leo Jumatatu na kutangazwa rasmi kama mchezaji wa Barcelona lakini kuanza kwake kucheza kunaweza kucheleweshwa kutokana na jeraha.

Nyota wa Barcelona Lionel Messi ametaka Philippe Coutinho kuwepo katika kikosi cha kwanza badala ya Ousmane Dembele. (Diario Gol)

Naby Keita

Liverpool watajaribu kumleta kiungo wa kati wa RB Leipzig na Guinea Naby Keita Anfield na wana nia ya kulipa zaidi kumpata mchezaji huyo wa miaka 22 mwezi Januari. (Telegraph)

Wing'a mbrazil Lucas Moura, 25, anataka kuondoka Paris St-Germain kujiunga na Manchester United mwezi huu. (Telefoot via Express)

Real Madrid inapanga kuwasajili Eden Hazard, 27 na kipa Thibault Courtois, 25, kutoka Chelsea ifikapo mwisho wa msimu. Lakini watasubiri kuona hatma ya Harry Kane wa Tottenham. (Sky Sports)

Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger anasema klabu yake haiko tayari kuongeza wachezaji zaidi Januari baada ya kumnunua kijana kutoka Ugiriki wa umri wa miaka 20, Konstantinos Mavropanos. (Sun)

Bournemouth wanatarajiwa kumsaini mfungaji bora zaidi wa Colchester United, Sammie Szmodics, 22, kwa gharama ya pauni milioni moja.

Kiungo wa kati wa Shakhtar Donetsk na Brazil Fred, 24, anasema anasubiri simu kutoka kwa meneja wa Manchester City Pep Guardiola. (GloboEsporte, kupitia Manchester Evening News)

Pep Guardiola

NewCastle wana matumaini ya kumaliza kumsaini wing'a wa Chelsea mbrazil Kenedy, 21. (Newcastle Chronicle)

Leicester City wakaribia kumsaini mchezaji wake wa kwanza mwezi Januari - mshambuliajo wa Mali Fousseni Diabate.

The Foxes wamekubalia pauni milioni 1.7 kwa mchezaji huyo wa miaka 22 ambaye anacheza ligi ya pili ya Ufaransa Gazelec Ajaccio. (Leicester Mercury)

Leeds United wamemurodhesha beki wa Brugge ya Ubelgiji Laurens de Bock, 25, kuwa lengo lake kuu. (Leeds Live)

Mwanariadha nguli Usain Bolt, 31, amesema atafanya majaribio na Borussia Dortmund mwezi Machi, lakini anatamani sana kuichezea Manchester United. (Express

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...