Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kansela Angela Merkel apokea tuzo ya 'Taa ya Amani'


Kansela wa Ujerumani Angela Merkel ametunukiwa tuzo ya Fransisca ya ā€˜'Taa ya Amani". Bibi Merkel amepewa tuzo hiyo kutokana na juhudi zake za kuhamasisha ushirikiano na amani miongoni mwa watu.




Wakati akipokea tuzo hiyo kansela wa Ujerumani Angela Merkel alisema njia ya amani na maridhiano mara nyingi hufaulu pale panapokuwa na jitihada na uvumilivu mwingi, na alisisitiza kuwa njia hiyo sio kizuizi cha imani ya kidini.


Akitolea mfano matatizo katika Umoja wa Ulaya unaojumuisha mataifa 28, bibi Merkel amesema ni muhimu kuangalia mbali zaidi ya upeo wa kitaifa, na kuongeza kuwa ni lazima uwepo uwezekano wa kuupa moyo Umoja wa Ulaya.

Kansela wa Ujerumani Angela Merkel

Kansela wa Ujerumani alielezea juu ya amani na jinsi inavyoendelea kuwa dhaifu duniani, akitolea mfano vita vya Balkans, iliyokuwa zamani Yugoslavia kwenye miaka ya tisini.Pia alizungumzia hatua ya Urusi ya kulitwaa jimbo la Crimea  mnamo mwaka 2014 pamoja na vita vya hivi karibuni vya wenyewe kwa wenyewe vya nchini Syria ambavyo amesema vimesababisha mgogoro mkubwa zaidi wa kibinadamu katika nyakati hizi za sasa. 

Kansela Merkel alizungumzia pia juu ya hatua ya rais wa Marekani Donald Trump ya kuiondoa nchi yake na kuiweka kando na mataifa makubwa kuhusiana na mkataba wa nyuklia wa Iran uliofikiwa mwaka 2015, maamuzi ambayo Merkel amesema yatalitumbukiza zaidi kwenye migogoro eneo la Mashariki ya Kati.

Rais wa Marekani Donald Trump

Tuzo hiyo ya "taa ya Amani"  ya Fransica ni mfano wa taa ya mafuta ya kioo inayowaka kwenye kaburi la mtakatifu Francis wa Assisi aliyeishi hadi mwaka 1226 na ambaye jitihada zake za kuwalinda wanyamapori zilihamasisha maadili ya kulinda mazingira.

Rais wa Colombia Juan Manuel Santos alipata tuzo ya amani ya Nobel na tuzo hiyo ya ā€˜Taa ya Amani' ya Francisca mnamo mwaka 2016 kutokana na jitihada zake zilizoleta upatanishi kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe vya nchini Colombia.

Rais wa Colombia Juan Manuel Santos

Tuzo hiyo ilitolewa kwa mara ya kwanza mwaka 1981 kwa kiongozi wa jumuiya ya wafanyakazi wa Poland Lech Walesa. Wapokeaji waliofuatia baadaye ni pamoja na Papa John Paul wa pili, Dalai Lama, Mama Teresa wa Calcutta na kiongozi wa kisiasa wa Urusi Mikhail Gorbachev.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...