Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Rouhani asema Marekani itajuta ikijitoa mkataba wa nyuklia


Rais Hassan Rouhani wa Iran amesema kwamba endapo Marekani itajiondoa kwenye mkataba wa nyuklia kati ya nchi yake na mataifa yenye nguvu duniani, basi Marekani itajutia maisha yake yote.



"Ikiwa Marekani itaondoka kwenye makubaliano ya nyuklia, mutaona hivi karibuni watakavyojutia kuliko ilivyowahi kuwatokezea kwenye historia," alisema mwanamageuzi Rouhani kwenye hotuba yake ya leo (Jumapili 6 Mei) akiwa kaskazini mwa Iran.


"Trump anapaswa kujuwa kuwa watu wetu wameunganika, utawala wa Kizayuni (Israel) unapaswa kujuwa kuwa watu wetu wako kitu kimoja," alisema Rouhani.

"Leo, mirengo yote ya kisiasa nchini Iran, ama iwe kulia au kushoto, wahafidhina, wanamageuzi na watu wa mrengo wa kati, wote wameungana," aliongeza.

Rais Donald Trump wa Marekani ametishia kujiondoa kwenye makubaliano hayo wakati utakapofika muda wa kusainiwa upya tarehe 12 Mei, akiwataka washirika wa Ulaya "kuyarekebisha makosa makubwa yaliyomo" ama sivyo arejeshe upya vikwazo dhidi ya Iran.

Mkataba huo wa nyuklia ulisainiwa mwaka 2015 kati ya Iran na Uingereza, China, Ufaransa, Ujerumani, Urusi na Marekani, wakati huo ikiongozwa na Barack Obama.

Chini ya makubaliano hayo, vikwazo vilipunguzwa kwa masharti ya Iran kutokuunda bomu la nyuklia, lakini Iran inasema haioni mafanikio ya ahadi hizo licha ya kutimiza masharti ya mkataba.

Mara kadhaa, Rouhani amekuwa akirejelea msimamo wa nchi yake kupinga kuzuiliwa nchi yake kuunda makombora yasiyo ya kinyuklia, na hilo amelizungumzia pia kwenye hotuba yake ya Jumapili.

Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa (kushoto) anaamini kuwa Marekani haina sababu ya kujitoa kwenye mkataba wa nyuklia wa Iran.

Naye Trump amekuwa akiukosoa mkataba huo, akitaja baadhi ya vifungu ambavyo anasema vinaondoa vikwazo vya nyuklia kuanzia mwaka 2025.

Macron aonya dhidi ya vita

Katika jitihada za kuyaokoa makubaliano hayo, Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa amependekeza hivi karibuni kwamba mkataba huo utanuliwe kuyashirikisha masuala kama hayo yanayolalamikiwa na Trumo, na pia kuondoa kikomo ya muda wa Iran kuruhusiwa kuunda makombora mengine na pia kuangalia dhima ya Iran kwenye eneo la Ghuba na Mashariki ya Kati.

Hatua ya Iran kumuunga mkono Rais Bashara al-Assad, kupitia kundi la Hizbullah la Lebanon, na pia kuwaunga mkono waasi wa Kishia nchini Yemen kumeongeza mzozo kati yake na mataifa ya Magharibi. 

Licha ya hayo, hivi leo Rais Macron ameonya kwamba kunaweza kuzuka vita endapo marekani itajiondoa kwenye makubaliano hayo. 

"Tunaweza kuibuwa mambo mengine mapya. Kunaweza kukawa na vita," Macron ameliambia gazeti la kila wiki la Ujerumani, Der Spiegel, ingawa ameongeza: "Sidhani kama Donald Trump anataka vita

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...