China yaitaka Korea Kaskazini kusitisha majaribio ya makombora
Pata kiungo
Facebook
X
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
-
MTEULE THE BEST Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionWang Yi anasema alimshauri Ri Yong-ho kuheshimu maazimio ya Umoja wa Mataifa wakati wa mkutano wao uliofanyika nchini Ufilipino.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa China amemuambia mwenzake wa Korea Kaskazini kuwa Korea Kaskazini itahitaji kusitisha majaribio ya makombora baada ya vikwazo vipya vilivyowekwa na baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa.
Wang Yi anasema alimshauri Ri Yong-ho kuheshimu maazimio ya Umoja wa Mataifa wakati wa mkutano wao uliofanyika nchini Ufilipino.
Hata hivyo hakusema vile bwana Ri alijibu.
Haki miliki ya pichaEPAImage captionWaziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Korea Kaskazini Ri Yong-ho
Siku ya Jumamosi baraza la usalama la Umoja wa mataifa, lilichukua hatua madhubuti ya kuiadhibu Korea Kaskazini kwa hatua yake ya mwezi uliopita ya kuifanyia majaribio zana zake za kitonoradi.
Katika kura ya pamoja, baraza hilo liliidhinisha vikwazo vipya, vinavyolenga biashara ya chuma na mkaa ya mawe ya Pyongyang ambayo huuza nje bidhaa hizo kwa zaidi ya dola bilioni kwa mwaka.
Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionKorea Kaskazini ikifanyia jaribio kombora
Rais wa Marekani Donald Trump, alipongeza hatua za China na Urusi za kuunga mkono vikwazo hivyo vilivyotolewa na baraza hilo la Umoja wa mataifa.
Anasema kuwa, vikwazo hivyo, vitakuwa na "athari kubwa mno" ya kibiashara.
Haki miliki ya pichaAFPImage captionKatika kura ya pamoja, baraza hilo liliidhinisha vikwazo vipya, vinavyolenga biashara ya chuma na mkaa ya mawe ya Pyongyang
Majirani wao Korea Kusini, wameiomba Korea Kaskazini kufuata njia ya mazungumzo, ili kutanzua mzozo uliopo wa mpango wa Pyongyang, kuhusu zana za kinuklia.
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni