China yaitaka Korea Kaskazini kusitisha majaribio ya makombora

MTEULE THE BEST
People"s Republic of China Foreign Minister Wang Yi gestures as he is escorted by Zhao Jianhua, Chinese ambassador to the Philippines, upon arrival at the international airport of Pasay to attend the 50th ASEAN Foreign Ministers meeting, metro Manila, Philippines August 5, 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionWang Yi anasema alimshauri Ri Yong-ho kuheshimu maazimio ya Umoja wa Mataifa wakati wa mkutano wao uliofanyika nchini Ufilipino.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa China amemuambia mwenzake wa Korea Kaskazini kuwa Korea Kaskazini itahitaji kusitisha majaribio ya makombora baada ya vikwazo vipya vilivyowekwa na baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa.
Wang Yi anasema alimshauri Ri Yong-ho kuheshimu maazimio ya Umoja wa Mataifa wakati wa mkutano wao uliofanyika nchini Ufilipino.
Hata hivyo hakusema vile bwana Ri alijibu.
North Korean Foreign Minister Ri Yong-ho arrives at a hotel in Manila, PhilippinesHaki miliki ya pichaEPA
Image captionWaziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Korea Kaskazini Ri Yong-ho
Siku ya Jumamosi baraza la usalama la Umoja wa mataifa, lilichukua hatua madhubuti ya kuiadhibu Korea Kaskazini kwa hatua yake ya mwezi uliopita ya kuifanyia majaribio zana zake za kitonoradi.
Katika kura ya pamoja, baraza hilo liliidhinisha vikwazo vipya, vinavyolenga biashara ya chuma na mkaa ya mawe ya Pyongyang ambayo huuza nje bidhaa hizo kwa zaidi ya dola bilioni kwa mwaka.
North Korea launches a Hwasong-14 missile, according to its KCNA news agency, in a photo dated 4 July, 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionKorea Kaskazini ikifanyia jaribio kombora
Rais wa Marekani Donald Trump, alipongeza hatua za China na Urusi za kuunga mkono vikwazo hivyo vilivyotolewa na baraza hilo la Umoja wa mataifa.
Anasema kuwa, vikwazo hivyo, vitakuwa na "athari kubwa mno" ya kibiashara.
North Korean labourers work beside the Yalu River at the North Korean town of Sinuiju on February 8, 2013 which is close to the Chinese city of Dandong. Piles of coal are seen.Haki miliki ya pichaAFP
Image captionKatika kura ya pamoja, baraza hilo liliidhinisha vikwazo vipya, vinavyolenga biashara ya chuma na mkaa ya mawe ya Pyongyang
Majirani wao Korea Kusini, wameiomba Korea Kaskazini kufuata njia ya mazungumzo, ili kutanzua mzozo uliopo wa mpango wa Pyongyang, kuhusu zana za kinuklia.
Beijing pia inaomba kurejelewa kwa mazungumzo

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

ZIJUWE SHERIA 17 ZA SOKA

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

KUMTUMAINIA MUNGU