Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ushindani mkali kati ya Odinga na Kenyatta matokeo Kenya

MTEULE THE BEST
Kuhesabu kura Mombasa
Kura zinaendelea kuhesabiwa katika vituo vingi
Kura zinaendelea kuhesabiwa na matokeo kutangazwa baada ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini Kenya Jumanne.
Katika matokeo yaliyokuwa yametangazwa kufikia saa sita unusu usiku, Uhuru Kenyatta wa chama cha Jubilee alikuwa akiongoza akiwa na kura 5,602,722 (55.22%) akifuatwa na Raila Odinga wa muungano wa upinzani National Super Alliance (Nasa) aliyekuwa na kura 4,462,244 (43.98%) Matokeo hayo ni ya vituo 27016 kati ya 253,637.
Kura ambazo zilikuwa zimeharibika kufikia wakati huo ni 247,051
Katika baadhi ya vituo, shughuli ya upigaji kura ilichelewa kuanza na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (IEBC) iliongeza muda kufikia wakati uliokuwa umepotezwa kabla ya kufungua vituo.
Kisheria, vituo vilitakiwa kufunguliwa saa kumi na mbili asubuhi na kufungwa saa kumi na moja jioni saa za Afrika Mashariki.
Lakini katika baadhi ya maeneo, mvua kubwa ilitatiza uchukuzi na upigaji kura na kwingine hitilafu za kimitambo zikachangia kukwamisha upigaji kura. Muda wa kufungwa kwa vituo uliongezwa kwa vituo vilivyochelewa kufunguliwa.
    Wengi wanahofia uwezekano wa kutokea tena kwa ghasia za baada ya uchaguzi sawa na ilivyotokewa baada ya uchaguzi wa mwaka 2007.
    Watu zaidi ya 1,100 walifariki na wengine 600,000 kuachwa bila makao.
    Ili kushinda, mgombea urais anahitajika kupata zaidi ya asilimia 50 ya kura zilizopigwa, na angalau asilimia 25 katika kaunti 24 kati ya kaunti 47 nchini humo.
    Iwapo hakuna mgombea atakayetimiza hilo, basi uchaguzi wa marudio utafanyika katika kipindi cha siku 30.

    Kujitokeza mapema

    Wapiga kura walianza kujitokeza alfajiri na mapema kupiga kura.
    Foleni ndefu zilishuhudiwa katika vituo vingi, na kwingine visa vya watu kuumia katika mkurupuko wa kupanga foleni vituo vilipofunguliwa viliripotiwa.
    Nairobi
    Watu walianza kupanga foleni nje ya vituo mapema
    Katika baadhi ya vituo, kuliripotiwa pia visa vya mitambo ya kuwatambua wapiga kura kufeli.
    Katika moja kati ya vituo vinne nchini humo, maafisa wa IEBC walikuwa wamesema kwamba hakuna huduma nzuri ya mtandao maana kwamba wasimamizi wa uchaguzi katika vituo hivyo watahitaji kusafiri hadi ameneo yenye huduma nzuri ya simu kutuma matokeo kikamilifu.
    Kumekuwa pia na taarifa kwmaba mwanamume mmoja ameuawa katika makabiliano kati ya wafuasi wa wagombea wawili katika kaunti ya Kilifi, pwani ya Kenya.
    Lakini kulikuwa na kisa cha kutia moyo pale mwanamke mmoja alipojifunzua mtoto msichana alipokuwa kwenye foleni akijiandaa kupiga kura Pokot Magharibi.
    Pauline Chemanang alisema kujifungua kwake ni baraka na akampa mtoto wake jina Kura, kwa mujibu wa kituo kimoja cha redio.
    Isinya, Kajiado, Nairobi, Kenya, 08 August 2017.
    Maafisa wa uchaguzi wanaendelea kuhesabu kura
    Uhuru Kenyatta Gatundu
    Bw Kenyatta amewahimiza Wakenya kudumisha umoja
    Raila Odinga
    Odinga amesema anahofia kwamba huenda kukatokea wizi wa kura
    Naibu Rais William Ruto akipiga kura katika kituo cha Kosachei, katika kaunti ya Uasin Gishu magharibi mwa Kenya
    Naibu Rais William Ruto akipiga kura katika kituo cha Kosachei, katika kaunti ya Uasin Gishu magharibi mwa Kenya
    Rais Kenyatta, baada ya kupiga kura yake kituo cha Mutomo eneo lake la nyumbani la Gatundu, kaskazini mwa Nairobi, alisema kwamba yuko tayari kukubali matokeo ya uchaguzi huo.
    "Kwa wapinzani wangu, kama nilivyosema mara nyingi awali, ikitokea kwamba washindwe, basi hebu tukubali uamuzi wa wananchi. Nina nia, mwenyewe, kukubali nia ya wananchi," amesema.
    Kiongozi wa upinzani Raila Odinga alipiga kura yake katika mtaa wa Kibera, Nairobi.
    Akiongea nje ya kituo hicho, aliwahimiza wafuasi wake: "Hebu tujitokeze kwa wingi na tupige kura."
    line break
    Mwangalizi mkuu wa Umoja wa Ulaya Marietje Schaake amesema itategemea sana imani ya wananchi katika mfumo mpya wa kiteknolojia wa kupiga kura.
    Kabla ya siku ya uchaguzi, meneja wa masuala ya teknolojia katika IEBC Chris Msando aliuawa na watu wasiojulikana.
      Kulikuwepo na madai ya kwamba huenda kukawa na wizi wa kura na pia katika baadhi ya maeneo taarifa za kueneza kwa karatasi zenye ujumbe wa chuki zilizagaa.
      Siku chache kabla ya uchaguzi, Wakenya wengi walikuwa wakinunua chakula na maji na kujihifadhia wakihofia hali baada ya uchaguzi.
      Polisi pia walifanya mipango ya kushughulikia dharura iwapo ghasia zingetokea.
      Wapiga kura kwenye foleni kaunti ya Uasin Gishu magharibi mwa Kenya
      Wapiga kura kwenye foleni kaunti ya Uasin Gishu magharibi mwa Kenya
      Gatundu
      Wapiga kura wakiwa kwenye foleni eneo la Gatundu

      Maoni

      Machapisho maarufu kutoka blogu hii

      MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

      Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

      Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

      MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

      Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

      Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...