Barcelona wanajiandaa kupanda dau kumtaka kiungo wa Tottenham Dele Alli, 21, baada ya kumuuza Neymnar kwa pauni milioni 200. (Sunday Express)
Bayern Munich wapo tayari kutoa pauni milioni 50 kumsajili kiungo wa Tottenham Eric Dier, 21. (Sun on Sunday)
Arsenal, Liverpool, Manchester City na Barcelona wanamtaka kiungo wa Monaco Thomas Lemar, 21. (Sunday Mirror)
Manchester United na Chelsea wanafikiria kumsajili kiungo wa Barcelona Sergi Roberto. (Don Balon)
Chelsea wanaonekana kuwa tayari kupambana vikali na Manchester United katika kumsajili Gareth Bale kutoka Real Madrid. (Sunday Express)
Barcelona wapo tayari kutoa pauni milioni 120 kumsajili kiungo mshambuliaji wa Liverpool Philippe Coutinho. (Star on Sunday)
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionPhilippe Coutinho
Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp tayari anapanga kutaka kumsajili Manuel Lanzini kutoka West Ham kuziba pengo la Philippe Coutinho. (Mundo Deportivo)
Antonio Conte amesema hana nguvu zozote za kuzuia Chelsea kumuuza Eden Hazard. (Sunday Mirror)
Barcelona wapo tayari kuwatoa Andre Gomes na Rafinha kama sehemu ya mkataba wa kumsajili Paulo Dybala kutoka Juventus. (Gazzetta dello Sport)
Everton wataamua kumfuatilia mshambuliaji wa Arsenal Danny Welbeck, 26, iwapo watashindwa kumshawishi Olivier Giroud, 30, kuondoka Emirates. (Sunday People)
Meneja wa Everton Ronald Koeman ana matumaini ya kumsajili beki wa zamani wa Arsenal Thomas Vermaelen, 31, kutoka Barcelona. (Sun on Sunday)
Arsenal wanaongoza katika mbio za kutaka kumsajili Lucas Moura kutoka Paris Saint-Germain. (UOL)
Real Madrid wamemhakikishia Gareth Bale, 28, kuwa bado ana nafasi katika klabu hiyo katika hatua ambayo pengine itawahuzunisha Manchester United. (Observer)
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionGareth Bale
Chelsea wana matumaini ya kuwazidi kete Liverpool katika kumsajili beki wa Southampton Virgil van Dijk, 26. (Evening Standard)
Meneja wa Juventus Massimiliano Allegri ameiambia Chelsea kuwa "hawana nafasi yoyote" na kumsajili beki kutoka Brazil Alex Sandro, 26. (ESPN)
Swansea lazima walipe pauni milioni 13 ikiwa wanataka kumsajili tena Wilfried Bony kutoka Manchester City. (Sunday Mirror)
Meneja wa Borussia Dortmund Peter Bosz amesema hana wasiwasi kuhusu kumpoteza mshambuliaji wake Ousmane Dembele, 20, anayenyatiwa na Barcelona. (Metro)
Barcelona wanamtaka kiungo wa kimataifa wa Ivory Coast Jean-Michael Seri, 26, anayechezea Nice, ambaye pia anasakwa na Arsenal. (Mundo Deportivo)
Image captionJean-Michael Seri
Matumaini ya Liverpool kumsajili kiungo wa Rennes, Benjamin Andre, 27, yamefifia. (Sunday Express)
Newcastle wanamtaka kipa wa West Ham Adrian, 30, ili kuimarisha safu yao ya makipa. (Sky Sports)
Mnunuzi ambaye bado hajafahamika kutoka China ameonesha nia ya kutaka kununua baadhi ya hisa za Manchester United. (Sunday Times)
Usikose kuungana nasi leo moja kwa moja kutoka Wembley kusikiliza mpambano wa Ngao ya Hisani kati ya Arsenal dhidi ya Chelsea. Kuanzia saa kumi alasini saa za Afrika Mashariki
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni