Rais wa Marekani Donald Trump amemshukuru Rais wa Urusi Vladimir Putin kwa kuagiza kuondoka kwa wafanyakazi 755 kutoka kwenye afisi za kibalozi za taifa hilo nchini Urusi.
Pata kiungo
Facebook
X
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
-
MTEULE THE BEST
Haki miliki ya pichaEPAImage captionUrusi imesema maafisa wa kibalo wa Marekani watatakiwa kuondoka kufikia tarehe 1 Septemba
Rais wa Marekani Donald Trump amemshukuru Rais wa Urusi Vladimir Putin kwa kuagiza kuondoka kwa wafanyakazi 755 kutoka kwenye afisi za kibalozi za taifa hilo nchini Urusi.
Akiongea na wanahabari New Jersey, kiongozi huyo amesema angependa kumshukuru sana kiongozi huyo wa Marekani kwa kuisaidia Marekani kuokoa fedha.
Uchunguzi unafanyika nchini Marekani kubaini iwapo kulikuwa na ushirikiano kati ya maafisa wa kampeni wa Trump na Urusi, inayodaiwa kuingilia uchaguzi mkuu wa mwaka 2016.
Bw Trump ameshutumu uchunguzi huo.
Mwishoni mwa mwezi Julai, Rais Putin alisema wafanyakazi 755 wangelazimishwa kuondoka kutoka afisi za kibalozi za Marekani nchini Urusi, akilipiza kisasi hatua ya Marekani kuiwekea Moscow vikwazo zaidi.
Wengi wa wafanyakazi hao ni waajiria wa kutoka Urusi, ikiwa na maana kwamba watu ambao watalazimishwa kuondoka nchini humo hawafiki 755.
Alisema watatakiwa kuondoka kufikia tarehe 1 Septemba, na kufikisha idadi ya wafanyakazi katika afisi za kibalozi wa Marekani hadi 455, sawa na wafanyakazi wa kibalozi wa Urusi walio Washington.
Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionPutin na Trump walikutana mjini Hamburg Ujerumani Julai
Shukrani
Wafanyakazi katika ubalozi wa Marekani mjini Moscow, pamoja na afisi za kibalozi katika miji ya Ekaterinburg, Vladivostok na St Petersburg wameathiriwa.
Wakati huo, wizara ya mambo ya nje ya Marekani ilitaja hatua hiyo kuwa ya kusikitisha na isiyofaa.
Lakini Bw Trump amemshukuru Bw Putin kwa kupunguza wafanyakazi wanaolipwa mishahara na serikali ya Marekani.
"Ningependa kumshukuru kwa sababu tunajaribu kupunguza wafanyakazi wetu na kwangu mimi namshukuru sana kwamba amewafukuza watu wengi kiasi hicho," amesema.
Aidha, Alhamisi, Rais Trump alisema alishangazwa sana na uvamizi uliofanywa katika nyuma ya mwenyekiti wake wa zamani wa kampeni Paul Manafort jimbo la Virginia na maafisa wa uchunguzi wa Marekani.
Mwanasheria maalum Robert Mueller, anayeongoza uchunguzi kuhusu tuhuma kwamba Marekani iliingilia uchaguzi wa Urusi, aliondoka nyumani kwa Manafort mjini Alexandria akiwa na "nyaraka kadha" kwa mujibu wa gazeti la Washington Post
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni