Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Rais wa Marekani Donald Trump amemshukuru Rais wa Urusi Vladimir Putin kwa kuagiza kuondoka kwa wafanyakazi 755 kutoka kwenye afisi za kibalozi za taifa hilo nchini Urusi.

MTEULE THE BEST
Ubalozi wa Moscow, Russia, on 28 Julai 2017Haki miliki ya pichaEPA
Image captionUrusi imesema maafisa wa kibalo wa Marekani watatakiwa kuondoka kufikia tarehe 1 Septemba
Rais wa Marekani Donald Trump amemshukuru Rais wa Urusi Vladimir Putin kwa kuagiza kuondoka kwa wafanyakazi 755 kutoka kwenye afisi za kibalozi za taifa hilo nchini Urusi.
Akiongea na wanahabari New Jersey, kiongozi huyo amesema angependa kumshukuru sana kiongozi huyo wa Marekani kwa kuisaidia Marekani kuokoa fedha.
Uchunguzi unafanyika nchini Marekani kubaini iwapo kulikuwa na ushirikiano kati ya maafisa wa kampeni wa Trump na Urusi, inayodaiwa kuingilia uchaguzi mkuu wa mwaka 2016.
Bw Trump ameshutumu uchunguzi huo.
Mwishoni mwa mwezi Julai, Rais Putin alisema wafanyakazi 755 wangelazimishwa kuondoka kutoka afisi za kibalozi za Marekani nchini Urusi, akilipiza kisasi hatua ya Marekani kuiwekea Moscow vikwazo zaidi.
Wengi wa wafanyakazi hao ni waajiria wa kutoka Urusi, ikiwa na maana kwamba watu ambao watalazimishwa kuondoka nchini humo hawafiki 755.
Alisema watatakiwa kuondoka kufikia tarehe 1 Septemba, na kufikisha idadi ya wafanyakazi katika afisi za kibalozi wa Marekani hadi 455, sawa na wafanyakazi wa kibalozi wa Urusi walio Washington.
Russian President Vladimir Putin and his US counterpart Donald Trump at the G20 summit in Hamburg, 7 July 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionPutin na Trump walikutana mjini Hamburg Ujerumani Julai

Shukrani

Wafanyakazi katika ubalozi wa Marekani mjini Moscow, pamoja na afisi za kibalozi katika miji ya Ekaterinburg, Vladivostok na St Petersburg wameathiriwa.
Wakati huo, wizara ya mambo ya nje ya Marekani ilitaja hatua hiyo kuwa ya kusikitisha na isiyofaa.
Lakini Bw Trump amemshukuru Bw Putin kwa kupunguza wafanyakazi wanaolipwa mishahara na serikali ya Marekani.
"Ningependa kumshukuru kwa sababu tunajaribu kupunguza wafanyakazi wetu na kwangu mimi namshukuru sana kwamba amewafukuza watu wengi kiasi hicho," amesema.
Aidha, Alhamisi, Rais Trump alisema alishangazwa sana na uvamizi uliofanywa katika nyuma ya mwenyekiti wake wa zamani wa kampeni Paul Manafort jimbo la Virginia na maafisa wa uchunguzi wa Marekani.
Mwanasheria maalum Robert Mueller, anayeongoza uchunguzi kuhusu tuhuma kwamba Marekani iliingilia uchaguzi wa Urusi, aliondoka nyumani kwa Manafort mjini Alexandria akiwa na "nyaraka kadha" kwa mujibu wa gazeti la Washington Post

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...