Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mourinho: Nitamsajili Gareth Bale akiuzwa

MTEULE THE BEST

Mshambuliaji wa Real Madrid Gareth Bale
Mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho anasema kuwa atakabiliana na makocha wengine kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Gareth Bale iwapo Real Madrid wanataka kumuuza.
Bale mwenye umri wa miaka 28 alijiunga na mabingwa hao wa Uhispania kwa fedha za uhamisho zilizovunja rekodi ya £85m kutoka Tottenham.
Mabingwa wa ligi ya Yuropa Man United wanakutana na Real Madrid ambao walishinda kombe la vilabu bingwa Ulaya katika kombe la Supercup Jumanne.
''Iwapo atashiriki ni ishara tosha kwamba atasalia Madrid'', alisema meneja wa Real Madrid
Mourinho alisema kuwa iwapo Bale atashiriki katika mechi hiyo basi atakuwa katika mpango wa kocha wake na klabu na ni haki na mpango wake kusalia.Basi sitafikiria kumpigania.
''Iwapo hayupo katika mpango wa klabu na ni kweli mchezaji kama Bale anataka kuondoka nitajaribu kuwa hapo nikimsubiri upande mwengine''.
Bale aliimarisha kandarasi yake katika klabu hiyo mwaka uliopita akisema anafurahi kusalia na mabingwa hao mara 12 wa kombe la vilabu bingwa.
TETESI ZA SOKA ULAYA JUMANNE 08.08.2017
Paris Saint-Germain wapo tayari kupanda dau kumtaka mshambuliaji wa Monaco, Kylian Mbappe, 18, na wanajiandaa kutoa pauni milioni 161 kumtaka mchezaji huyo anayesakwa pia na Real Madrid na Manchester City. PSG watamuuza Angel Di Maria ili kupata fedha zaidi za kukamilisha usajili huo. (Le Parisien)

Liverpool watapanda dau la pauni milioni 60 kumtaka Virgil van Dijk kufuatia hatua ya mchezaji huyo kuwasilisha rasmi maombi ya kutaka kuondoka Southampton. Chelsea pia wanamtaka beki huyo, ingawa Antonio Conte anataka zaidi kusajili mabeki wa pembeni huku Serge Aurier wa PSG akiwa miongoni mwao. (Express)

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho ameghadhibishwa na matatizo ya beki wa PSG Serge Aurier ya kupata kibali cha kufanya kazi Uingereza, na hivyo kuamua kuelekeza nguvu zake kumtaka Fabinho wa Monaco na anadhani dau la pauni milioni 45 litatosha kumshawishi. (Don Balon)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp atakataa mkataba wowote kuhusu Philippe  Coutinho kuondoka Anfield kwenda Barcelona. (Daily Mirror)

Liverpool hawataweza kumzuia Philippe Coutinho, 25, kuondoka msimu huu amesema mkongwe wa klabu hiyo Greame Souness. (Sky Sports)

Mshambuliaji wa zamani wa kimataifa wa England Ian Wright amesema Philippe Coutinho ā€œhana budi kwendaā€ Barcelona. (BBC Radio 5 Live)

Barcelona bado wanataka kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Ousmane Dembele, 20. (Sport)

Manchester United watapanda dau kutaka kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Gareth Bale, 28, ikiwa mchezaji huyo ataachwa na Zinedine Zidane katika kikosi kitakachocheza fainali ya Uefa Super Cup. (Times)

Meneja wa Real Madrid Zinedine Zidane ametupilia mbali taarifa za Gareth Bale kurejea England. (Mirror)

Chelsea na Manchester United zote zitapanda dau kumtaka beki wa PSG Serge Aurier, 24. (Daily Mail)

Kiungo wa Leicester City Danny Drinkwater anajiandaa kuiambia klabu yake kuwa anataka kuondoka na kujiunga na Chelsea. (Mirror)

Eden Hazard yuko  tayari kuondoka Chelsea na kujiunga na Real Madrid. (Don Balon)

Chelsea wana matumaini makubwa ya kumpata beki wa Southampton Virgil van Dijk kwa sababu ya uhusiano tete kati ya Liverpool na Southampton. (Telegraph)

Southampton wanapanga kumsajili beki wa kati wa Middlesbrough Ben Gibson, 24, kuziba nafasi ya Virgil van Dijk. (Sun)

Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal, Ian Wright amesema Arsenal walitakiwa kumsajili Nemanja Matic kutoka Chelsea kwa sababu timu hiyo inakosa kiongozi uwanjani. (BBC Radio 5 Live)

Manchester United na Inter Milan zimerejea tena kumtaka beki wa kushoto wa Tottenham Danny Rose, 27. (Daily Mirror)

Manchester City wamemuulizia kiungo wa Barcelona Sergio Busquets. (Onda Cero)

Valencia wanajiandaa kupanda dau la kumshawishi beki wa Arsenal Gabriel, 26, kuhamia Uhispania. (Evening Standard)

Trabzonspor ya Uturuki inataka kumsajili kiungo wa Tottenham Moussa Sissoko, 27, kwa mkopo. 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...