Arsenal wamempa Alexis Sanchez mkataba mpya na mshahara wa pauni 300,000 kwa wiki na kumfanya mchezaji anayelipwa zaidi katika EPL. (Daily Mail)
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amekiri kuwa "hana uhakika sana" kama ataweza kumshawishi Alexis Sanchez kukubali kusaini mkataba mpya. (SFR)
Juventus wanajiandaa kutoa pauni milioni 23 kujaribu kuishawishi Liverpool kumuuza Emre Can. (Gazzetta dello Sports
Juventus nao wameingia katika mbio za kutaka kumsajili Sergi Roberto kutoka Barcelona, ambaye pia Manchester United na Chelsea zinamtaka. (Sport.es)
West Ham wamepanda dau la pauni milioni 27.1 kumtaka kiungo wa Sporting Lisbon William Carvalho, 25. (Daily Telegraph)
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionLiverpool hawataki kumuuza Philippe Coutinho kwa Barcelona
Barcelona hawatakuwa na uwezo wa kumnunua Philippe Coutinho kutoka Liverpool iwapo watafanikiwa kumsajili Ousmane Dembele, 20, kutoka Borussia Dortmund, kwa mujibu wa mwandishi wa ha1ba12ri za michezo Graham Hunter. (BBC Radio 5 Live)
Barcelona wapo tayari kuwapa Liverpool Ivan Rakitic kama sehemu ya mkataba wa kumsajili Philippe Coutinho. (Don Balon)
Barcelona wanamtaka kiungo mchezeshaji wa Real Madrid Marco Asensio na wapo tayari kutoa pauni milioni 72. (Diario Gol)
Mwenyekiti wa Tottenham Daniel Lexy anakabiliwa na sekeseke la wachezaji kudai kuongezewa mishahara baada ya beki Danny Rose kushutumu sera za klabu hiyo. (Daily Mirror)
Danny Rose alipokelewa kwa shangwe na wachezaji wenzake baada ya kuweka wazi mtazamo wa Tottenham, huku wachezaji wengine wakitishia na wao kuweka mambo hadharani. (Daily Mirror)
Wachezaji nyota wa Tottenham wanataka kuondoka kwa sababu ya sera ya malipo ya klabu hiyo. (Daily Mail)
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionDanny Rose alifunga mabao 18 Ligi ya Premia msimu uliopita
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho anatafuta beki wa kushoto na Danny Rose wa Tottenham ni mmoja wa wachezaji anaowafuatilia. (Daily Record)
Meneja wa Everton Ronald Koeman ameiambia Tottenham kuwa hawataweza kumsajili kiungo Ross Barkley kwa bei rahisi. (Daily Star)
Arsenal wanaamini kuwa wamefanikiwa katika mazungumzo ya kumshawishi Mesut Ozil kubakia Emirates baada ya kumpa mkataba wa mshahara wa pauni 225,000 kwa wiki, na mchezaji huyo ameonesha dalili za kukubali. (Sun)
PSG wapo tayari kuwapa Atletico Madrid Javier Pastore katika mkataba wa kumsajili kipa Jan Oblak, 24. (AS)
Real Madrid wamekuwa na mazungumzo ya siri na Juventus kuhusiana na mshambuliaji Paulo Dybala, 23, ambaye pia anasakwa na Barcelona. (Don Balon)
Juventus wanamtaka Kevin Strootman kabla ya dirisha la usajili kufungwa, huku Roma wakisema bei yake ni euro milioni 45. (Tuttosport)
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Arsene Wenger amesema meneja wa Chelsea Antonio Conte awarejeshe wachezaji wanaocheza nje kwa mkopo kama ana wasiwasi na dogo wa kikosi chake. (Times)
Msimu wa EPL unaanza rasmi leo. Arsenal wanacheza na Leicester City saa nne kasorobo usiku huu kwenye uwanja wa Emirates.
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni