Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MTWA MKWAWA: KIONGOZI WA WAHEHE ALIYEKUWA MLUGURU KWA ASILI

MTEULE THE BEST



Wengi tunajua kuwa alikuwa mhehe, ila leo nawaletea makala hii yenye kuchokoza mjadala juu ya Asili ya Chief Mkwawa.
ā€¦ā€¦ā€¦ā€¦ā€¦ā€¦ā€¦ā€¦ā€¦ā€¦ā€¦ā€¦ā€¦ā€¦
Mtwa Mkwawa hakuwa Mhehe na wala hakuwa mtoto wa Mnyigumba (kama historia iliyoandikwa na Wajerumani na inapotosha); bali Mkwawa alikuwa ni mtoto wa dada yake Mnyigumba ambaye aliolewa na Mtemi wa Waluguru. Hivyo Mkwawa alikuwa Mluguru kwa asili.
Akiwa mdogo alikwenda kumtembelea mjomba wake (Mnyigumba) na kutokana na ushujaa wake, Mkwawa alishiriki kupiga vita vikali dhidi ya Wangoni pale Makambako. Mnyigumba akampenda Mkwawa kuliko watoto wake, na ndio chanzo cha kupewa urithi pamoja na mtoto wa Mnyigumba aliyeitwa Muhenga. Ndio maana Muhenga (mtoto orijino wa Munyigumba), akawa na bifu kali na Mkwawa na bifu hilo halikuisha hadi Muhenga alipofariki!
Sherehe za kuapishwa Mtwa Mkwawa zilifanyika Dodoma eneo la Mpwapwa. Sherehe hizo zilihudhuriwa na wajomba zakeā€”Mtemi  Mazengo, Kimweri, Lugulu na Mirambo. Inasemekana wakiwa katika kushangilia na kuimba, ā€œMpwa! Mpwa!ā€ na ndipo neno Mpwapwa likazaliwa.
Mtwa Mkwawa alikuwa na vikosi vinne vya jeshi la vita; kimojawapo kilikuwa cha upelelezi na ushambuliaji (Kiitwacho Vamalavanu) ambacho kilikuwa kikila nyama ya mbwa ikichanganywa na dawa ya tambiko. Wahehe waliamini kuwa watakuwa na uwezo wa kunusa maadui na wao kutoonekana. Hivi ndivyo ulaji nyama ya mbwa ulivyoanza huko Uheheni na sharti ilikuwa kwamba mchuzi wa mbwa unywewe ukingali wa moto!
Mtwa Mkwawa alijua kusoma na kuandika kwa ufasaha lugha ya Kiarabu na alikuwa muumini wa dini ya Kiislamu. Mambo yalipokuwa magumu, Mtwa Mkwawa aliandika barua ya kwenda kwa Wajerumani akiwaomba wampe (upenyo) wa kuwashambulia makabila ya Wabena na Wakinga ambao walijisalimisha na kupatana na Wajerumani.
Watafiti tunajiridhisha kwamba hii ilikuwa ishara ya Mtwa Mkwawa kukata tama, maana isingekuwa rahisi kwa Wajerumani kumruhusu kufanya alichotaka.
Mtwa Mkwawa hakujipiga risasi, bali alijitumbukiza katika daraja la Kikongoma lililopo Mto Ruahaā€”mahali ambapo mama yake mzazi pia alijitumbukiza na kujiua pale. Lile fuvu linalodaiwa kuwa ni la Mtwa Mkwawa,  halikuwa lake ila inadaiwa kwamba ni fuvu la mlinzi wake. Hadi leo hakujawahi kufanyika DNA na kuthibitisha fuvu hilo.
Kwenye vita iliyomsambaratisha Mtwa Mkwawa, Wajerumani walifanikiwa kumkamata mdogo wake aliyeitwa Mpangile. Walimtundika kitanzini lakini hakufa, wakampiga risasi, hakufa! Baadae akatoboa siri kuwa wammwagie maji na wamchome mkuki-ndipo atakufa!
Baada ya kuona hivyo Wajerumani wakampa jina ā€œMpangelwangindo Mgopisala Sasisinagopiā€ikiwa na maana ya Mpangile anaeogopa mkuki risasi haogopi. Hapo walipomuulia Mpangile panaitwa Kitanzini mpaka leo!
Kutokana na kuwa Mluguru kwa asili, ndio maana Mtwa Mkwawa alikuwa na uhusiano wa karibu na Mtemi Mazengo (Ugogo Dodoma), pamoja na Mtemi Mirambo wa Unyamwezini Tabora. Mazengo, Mirambo na Mtemi wa Uluguru, walikuwa ndugu wa damu na walikuwa wajomba wa Mkwawa. Tunaambiwa hata wakati wa kurejesha fuvu linalodaiwa kuwa la Mtwa Mkwawa kutoka Ujerumani, na kuliweka kwenye Makumbusho ya Mkwawa pale Kalenga, Wagogo walimiminika kutoka Dodoma kwa wingi sana na walikuwa wakiimba na kucheza kwa bidii na kwa nguvu kupita hata Wahehe wenyewe!
Mtwa Mkwawa alikuwa na rada za asili alizozitega milimani ambazo zilikuwa zikimjulisha hali ya vita na ujio wa maadui katika himaya yake. Rada hizo zilizoitwa ā€œVimwanyulaā€, zilipoangushwa na Wajerumani ndio ulikuwa mwanzo wa kushindwa kwa Mtwa Mkwawa katika vita. Siku Vimwanyula vilipoanguka kwa mashambulizi ya Wajerumani, Wahehe walilia hivi: ā€œFimwanyula figwe, Ililinga lyavembile dandaā€ wakimaanisha; ā€œRada  zimeanguka na sasa Iringa inalia machozi ya damuā€
Mkuu wa Kikosi cha Usalama wa Ufalme wa Mtwa Mkwawa aliyeitwa Chavala, ndie aliesababisha anguko la Mkwawa mbele ya Wajerumani baada ya kuanika siri zote za kijeshi, kimizimu na kiganga alizokuwa akitumia Mkwawa. Chavala alishawishika kumuasi Mkwawa baada ya kupewa rupia 5,000 na Wajerumani.
Mtwa Mkwawa alikuwa na zake 63, waliokuwa wakiishi Ipamba na mamia ya watoto aliowajengea makazi eneo la Tosamaganga. Kwa sasa Ipamba pamejengwa Hospitali na Tosamaganga kuna shule na misheni.
Historia inayofundishwa shuleni na vyuoni kuhusu Mtwa Mkwawa na ambayo iliandikwa na wakoloni, imepindishwa sana. Wajerumani walikipata cha mtema kuni na kwa jeuri na kwa makusudi, hawajaingiza matendo na mambo mengi sana ya kishujaa aliyofanya Mtwa Mkwawa.
Mathalani, kwenye historia, Wajerumani wanasema askari wao waliouawa na jeshi la Mkwawa pale Lugalo, walikuwa mia tatu (300), lakini wazee walinieleza kwamba askari wa Kijerumani waliofariki pale walikuwa zaidi ya elfu tano!
Naamini umepata japo kitu na itakuamsha kuwa mtafiti kwa mambo unayofundishwa ama kuambiwa ama kusoma.
Mie najiuliza, ikiwa historia inayotuzunguka kama ya Mtwa Mkwawa wameipindisha namna hii, je, hayo masomo mengine kuna pumba ngapi zimeingizwa humo? Maana masomo mengi na mitaala yetu shuleni na vyuoni tumeikopi na kupesti kutoka kwao! Nina wasiwasi, mfumo wa elimu yetu unazalisha wasomi vibogoyo ambao, badala ya kutawala mazingira, wananyanyaswa na mazingira.

Makala hii imeandaliwa na Ndugu, Albert Nyaluke Sanga.

Kama una ushaidi juu ya asili ya Mkwawa wa Uhehe, tuwasiliane! Ni wakati wa kuandika historia yetu na kuacha historia iliyopindishwa na wakoloni na vijibwa vyao.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...