Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Justin Gatlin amshinda Usain Bolt mbio za mita 100

MTEULE THE BEST
Gatlin
Justin Galtlin amshinda Usain Bolt mbio za mita 100
Justin Gatlin alizima matumaini ya Usain Bolt ya kustaafu kutoka riadha akiwa kileleni aliposhindwa wakati wa mbio za mita 100 kwenye mashindano ya IAAF mjini London.
Bolt alimaliza mbio hizo katika nafasi ya tatu na kushinda shaba huku Christian Coleman mwenye umri wa miaka 21 akichukua nafasi ya pili.
    Gatlin mwenye umri wa miaka 35 ambaye alipigwa marufuku mara mbili alikimbia laini ya saba kwa muda wa sekunde 9.92.
    Final result
    Matokeo
    Gatlin bingwa wa mita 100 mwaka 2004 na bingwa mara mbili mwaka 2005, alikuwa amekemewa na umati wakti wote kila mara kufuatia historia yake ya kupigwa marufu kwa kutumia dawa za kuongeza nguvu za mwili.
      Baada ya kugunduliwa mara ya pili mwaka 2006 aliponea kupigwa marufuku maishani alipokubali kushirikiana na mamlaka na kukubali marufuku ya miaka minane ambayo baadaye ilipunguzwa hadi miaka minne baada ya kukata rufaa.
      Bolt beaten by Coleman
      Bolt (kushoto) na Coleman (kulia)
      Hatua hiyo ilimruhusu kurejea tena mbioni.
      Hata hivyo umati ulijibua kwa kumshangilia Usain Bolt wakati matokeo yalipotokewa hiyo jana.
      Bolt mwenye umri wa miaka 30 hajawai kupoteza mbio za mita 100 katika ubingwa wa dunia.
      Gatlin last won a major individual title in 2005 and had only beaten Bolt once before
      Bolt akimpongeza Gatlin

      Maoni

      Machapisho maarufu kutoka blogu hii

      MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

      Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

      Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

      MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

      Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

      Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...