Madaktari wapigana ndani ya chumba cha upasuaji, India
Pata kiungo
Facebook
X
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
-
MTEULE THE BEST Image captionMadaktari wanaonekana wakitukanana kwa Kihindi
Picha ya madaktari wawili wakipigana wakati walipokuwa wakimfanyia mgonjwa upasuaji, imesambaa katika mitandao ya kijamii
Madaktari hao wawili wamesimamishwa kazi kwa muda nchini India, baada ya video kusambaa mitandaoni wakigombana vikali, huku wakiwa wamesimama kandokando ya mama mmoja mja mzito, wakati wa upasuaji.
Taarifa kutoka Hospitali hiyo imethibitisha kuwa wawili hao wamesimamishwa kazi kwa muda.
Video ya kisa hicho kilichotokea katika Hospitali ya Umaid iliyoko kaskazini mwa mji wa Rajasthan, imesambazwa pakubwa na kusababisha malalamishi makubwa.
Afisa mmoja mkuu wa Hospitali hiyo ameiambia BBC kuwa, mwanamke aliyekuwa akifanyiwa upasuaji na mwanawe wako salama.
Chanzo cha video hiyo bado haijabainika, lakini wakuu wamethibitisha kuwa kisa hicho kilifanyika hospitalini humo.
Matusi mtandaoni
Mara baada ya kuonekana kwa mkanda huo wa video mtandaoni, ripoti nyingi ilidai kuwa mwanamke anayeonekana akiwa katika meza ya upasuaji alimzaa mtoto ambaye alifariki baadaye.
Lakini Dkt Ranjana Desai, mkuu wa Hospitali hya Umaid mjini Jodhpur, amekanusha madai hayo na kusema mtoto na mamake wako salama u salmini.
''Wakati nilipoina video hiyo, na kufanya uchunguzi wa ndani kwa ndani, vyombo vya habari tayari vilikuwa vimetangaza kuwa, mtoto huyu alikuwa amefariki," ameiambia BBC.
Kuna mtoto amefariki lakini siye ambaye vyomo vya habari vilitangaza, amesema.
Mita chache kutoka hapo, kwenye meza nyingine ya upasuaji, kwenye chumba hicho hicho hospitalini, mama mwingine alizalishwa mtoto ambaye alikuwa amefariki tayari.
"Visa hivi viwili havina uhusiano hata kidogo," Dkt Desai ameiambia BBC.
Kwenye Video, ambayo imesambazwa pakubwa mitandaoni, madaktari wawili wanasikika wakirushiana matusi mazito mazito kwa lugha ya Kihindi, na kuanza baadaye kugombana ikiwa mgonjwa huyo alikuwa amekula kabla ya upasuaji.
Dkt Desai amewatambua madaktari hao wawili na kutaja majina yao kama Dkt Ashok Nanival na Dkt Mathura Lal Tak.
Amesema kuwa madaktari hao hawajafutwa kazi bali wamesimamishwa tu kazi kwenye Hospitali hiyo, huku mamlaka kuu ya Hospitali hiyo ikiendeleza uchunguzi dhidi ya kisa hicho.
Mahakama kuu ya jimbo la Rajasthan imeamuru Hospitali hiyo kutoa ripoti ya kina, huku mahakama hiyo ikitekeleza uchunguzi wao kuhusiana na kisa hicho.
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni