Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Marekani: Tutaendelea na mazungumzo na Korea Kaskazini

MTEULE THE BEST
Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong-un na mwenzake wa Marekani Donald Trump
Image captionRais wa Korea Kaskazini Kim Jong-un na mwenzake wa Marekani Donald Trump
Waziri wa ulinzi nchini Marekani James Mattis amesema kuwa Marekani itaendelea na mazungumzo ya kidiplomasia na Korea Kaskazini.
Matamshi hayo yanajiri baada ya rais Donald Trump kusema katika mtandao wake wa Twitter kwamba mazungumzo sio suluhu kwa mipango ya kijeshi ya Korea Kaskazini.
Urusi pia imeionya Marekani dhidi ya kuchukua hatua za kijeshi akisema madhara yake yatakuwa makubwa.
Korea Kaskazini ilizuwa wasiwasi baada ya kurusha kombora kupitia anga ya Japan siku ya Jumanne.
Kombora hilo ambalo Japan limelitaja kuwa tishio lisilo la kawaida , lilivuka katika anga ya kaskazini ya kisiwa cha Japana cha Hokkaido mapema siku ya Jumanne, na kusababisha raia kujificha kabla ya kombora hilo kuanguka baharini yapata kilomita 1,180 .
Korea Kaskzini baadaye ilisema kuwa ni hatua mojawapo ya operesheni zake za kijeshi katika eneo la pacific na kurejelea tishio lake la kushambulia kisiwa cha pacific cha Guam.
Waziri wa ulinzi nchini Marekani James Mattis
Image captionWaziri wa ulinzi nchini Marekani James Mattis
Siku chache zilizopita, bwana Trump alikuwa amenukuliwa akisema anaamini kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong un alikuwa ameanza kuheshimu Marekani.
Lakini katika chapisho lake la siku ya Jumatano , alisema: Marekani imekuwa ikizungumza na Korea Kaskazini na kuwalipa fedha kwa miaka 25.
''Kuzungumza nao sio suluhisho''.lakini alipoulizwa iwapo ni kweli kwamba Marekani imepoteza matumaini ya kidiplomasia , bwana Mattis alitofautiana wazi na rais Trump akisema: Hapana. Sisi hatujapoteza matumaini kupitia kutatua maswala kidiplomasia .
Alikuwa akizungumza alipokutana na mwenzake wa Korea Kusini Song, Young-moo katika Pentagon.
''Tunaendelea kufanya kazi pamoja na waziri na mimi tunagawana majukumu ili kulinda mataifa yetu, idadi yetu na maslahi yetu

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...