Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionKiungo wa kati wa Ujerumani Julian Draxler
Arsenal wanafanya jaribio la dakika za mwisho kumsajili mshambuliaji wa Paris St-Germain Julian Draxler, 23, na wakimkosa watazuia uhamisho wa Alexis Sanchez, 28, kwenda Manchester City. (Daily Mirror)
Manchester City watapanda dau la pauni milioni 70 taslimu kutaka kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28, na tayari wamepeleka kikosi chake cha wansheria na madaktari nchini Chile kwa ajili ya kukamilisha usajili huo. (Independent)
Matumaini ya Manchester City ya kumsajili beki wa West Brom Jonny Evans, 29, bado ni ati ati, kwa sababu Eliaquim Mangala, 26, ambaye angehusika katika mkataba huo hataki kwenda West Brom.
Arsenal na Leicester walipanda dau la pauni milioni 25 kumtaka beki huyo, lakini maombi yao yalikataliwa. (Daily Telegraph)
Crystal palace wana matumaini ya kumsajili Eliaquim Mangala kutoka City kwa pauni milioni 23. (Sun)
Swansea wanakaribia kumsajili kiungo wa Bayern Munich Renato Sanches kwa mkopo. (Guardian)
Haki miliki ya pichaREX FEATURESImage captionEliaquim Mangala
West Ham wanapanga kumchukua Jack Wilshere, 25, kwa mkopo kutoka Arsenal. (Sun)
Baada ya kukosa mtu wa kumsaidia Victor Moses, Chelsea wanafikiria kumsajili Bacary Sagna. (Daily Star)
Mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa, 28, anakaribia kujiunga tena na Atletico Madrid ambao wametoa dau jipya la pauni milioni 49 ambazo Chelsea wanafikiria kuzipokea. (Sun)
Chelsea bado wapo kwenye mazungumzo na Everton ya kumsajili kiungo mshambuliaji Ross Barkley, 23, huku muda ukizidi kutaradad wa kusajili wachezaji watatu wapya ambao Antonio Conte aliwataka. (Daily Telegraph)
Tottenham pia wanafikiria kumsajili Ross Barkley. (Evening Standard)
Tottenham wanaongoza katika mbio za kutaka kumsajili winga wa Leicester City Demarai Gray kabla ya dirisha la usajili kufungwa leo. (Daily Mirror)
Tottenham wanajiandaa kukamilisha usajili wa beki wa kulia wa PSG Serge Aurier, 24, kwa pauni milioni 23 baada ya wizara ya mambo ya ndani ya Uingereza kumpa kibali cha kufanya kazi. (Guardian)
Barcelona, Chelsea na Tottenham zinamnyatia winga wa Leicester City Riyad Mahrez, 26. (L'Equipe)
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionLemar aliwasaidia Monaco kushinda Ligue 1 msimu uliopita
Chelsea wapo kwenye mazungumzo ya kina na Swansea ya kumsajili mshambuliaji Fernando Llorente, 32. (ESPN)
Everton wanafikiria kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Mitchy Batshuayi. (FootMercato)
Liverpool wanaendeleza juhudi zao za kumsajili kiungo wa Monaco Thomas Lemar, 21, na wamepanda dau la pauni milioni 74. (Independent)
Liverpool tayari wameandaa madaktari kusafiri kwenda Paris kwa ajili ya vipimo vya afya vya Thomas Lemar, wa Monaco, iwapo makubaliano yatafikiwa baina ya timu hizo mbili. (Liverpool Echo)
Liverpool pia wapo tayari kutoa pauni milioni 75 kumsajili beki wa kati wa Southampton Virgil van Dijk, 26, ingawa Southampton wamesema hawataki kumuuza. (Times)
Meneja wa Newcastle anataka kumsajili mshambuliaji wa Liverpool Divock Origi, kuziba nafasi ya Dwight Gayle ambaye anataka kuondoka. (Express)
Fulham wamepanda dau la pauni milioni 15 kumtaka mshambuliaji wa Newcastle Dwight Gayle, 27, lakini Newcastle wanataka pauni milioni 18-20. (Daily Mail)
Newcastle wanatarajiwa kuwa na pilikapilika nyingi leo kabla ya dirisha la usajili kufungwa huku wakitaka kumsajili kwa mkopo winga wa Chelsea Kenedy, 21. (Evening Chronicle)
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionVirgil van Dijk amechezea Uholanzi mechi 12
Tottenham na West Ham wapo tayari kupambana kumsajili kiungo wa Barcelona Andre Gomes, 24. (Daily Mirror)
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni