Swahili navigation Yaliyomo Je wajua ndege hutumia harufu kusafiri maeneo ya mbali?
Pata kiungo
Facebook
X
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
-
MTEULE THE BESTHaki miliki ya picha
B. G. THOMSON/SCIENCE PHOTO LIBRARYImage captionNdege kwa jina Arctic turn uhamia maeneo yalio umbali wa maelfu ya kilomita bila kupotea.
Ndege uhamia maeneo yalio umbali wa maelfu ya kilomita bila kupotea.
Kwa mfano ndege kwa jina Arctic yeye huwa Uingereza majira ya joto na baadaye kusafiri hadi eneo la Atarctic wakati wa majira ya baridi.
Licha ya hayo yote kufanyika , wanasayansi bado hawajui ni vipi ndege husafiri kwa umbali huo wote na kuwasili katika maeneo wanayoelekea kila mwaka bila kupotea.
Kulingana na utafiti mpya, harufu hutumika kama kiungo muhimu wakati ndege hao wanapohamia maeneo mengine yalio mbali wakiwa juu ya bahari.
Watafiti kutoka chuo kikuu cha Oxford, Barcelona na Pisa kwa makusudi waliwatoa viungo vya mwili vinavyobaini harufu ndege hao kabla ya kufuatilia wanakoelekea.
Walibaini kwamba wanaweza kusafiri juu ya ardhi lakini wanaonekana kupotea wanapopaa juu ya bahari.
Hatua hiyo ilibaini kwamba hulazimika kutumia ramani ya harufu kutafuta njia ya wanakoelekea wakati ambapo hawaoni cha kutegemea.
Vipimo vya awali vilionyesha kuwa unapowatoa ndege hao viungo wanavyotumia kutambua harufu unawazuia kuweza kurudi walikotoka.
Hatahivyo wengine walikuwa na maswali ya iwapo unapowatoa viungo hivyo unaweza kulemaza uwezo wao wa kutafuta chakula.
Utafiti mpya unaondosha pingamizi hizo, na kuonyesha kuwa itakuwa vigumu katika siku za usoni kuhoji kwamba hatua ya kutambua harufu haitumiki wakati ndege hao wanaposafiri maeneo ya mbali ,alisema mtafiti Oliver Padget wa idara ya elimu ya wanyama katika chuo kikuu cha Oxford.
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni