Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Umoja wa Mataifa wataka machafuko ya Myanmar kusitishwa

MTEULE THE BEST

Katibu wa Umoja wa Mataifa amesema kampeni ya kijeshi ni sawa na takasataka ya kikabila dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya.
Bangladesch FlĆ¼chtlingslager Kutupalong (Getty Images/AFP/M. Uz Zaman)
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limevunja kimya chake kirefu kuhusu mgogoro wa nchini Myanmar na kutoa wito wa kukomesha vurugu, huku Katibu wa Umoja wa Mataifa akisema kampeni ya kijeshi ni sawa na takasataka ya kikabila dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya. Wakati huohuo, shirika la habari la serikali ya Myanmar limesema China imeunga mkono hatua za jeshi la Myanmar dhidi ya wapiganaji wa Rohingya.
Kwa mara ya pili, Baraza la Usalama lenye wanachama kumi na tano lilikutana faraghani kujadili mzozo wa Myanmar na wakakubali kwa pamoja kulaani hali hiyo hadharani. Tekeda Alemu, rais wa sasa wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na balozi wa Ethiopia katika Umoja wa Mataifa amesema: "Baraza limeelezea wasiwasi kuhusu ripoti za matumizi ya vurugu kupita kiasi wakati wa operesheni za usalama, na kutaka usitishwaji wa mara moja wa machafuko hayo ili irudishe hali ya kawaida ya kuzingatia sheria, kuhakikisha raia wanalindwa na kusuluhisha tatizo la wakimbizi."
Changamoto kuu kwa Aung San Suu Kyi
Myanmar Aung San Suu Kyi Rede vor der UN Vollversammlung in New York 2016 (Reuters/C. Allegri)
Machafuko ya Rakhine na kukimbia kwa maelfu ya wakimbizi, ni changamoto kubwa kuwahi kumkabili kiongozi wa Myanmar ambaye pia ni mshindi wa tuzo la Amani Aung San Suu Kyi tangu awe kiongozi wa taifa hilo mwaka uliopita.
Mapigano hayo yalianza kufuatia misururu ya mashambulizi ya wanamgambo wa Rohingya dhidi ya vituo vya kiusalama mnamo Agosti 25, ambapo watu kadhaa waliuawa. Abdul Goffar ambaye ni mmoja kati ya wakimbizi wa Rohingya anaelezea masaibu yaliyowakumba: "Wakati wanajeshi na polisi walipokizingira kijiji chetu na kutushambulia kwa maroketi kuwasha moto, tulikimbia kutoka kijiji chetu na kuelekea kokote kule tulikoweza kwenda."
Hata hivyo balozi wa China nchini Myanmar Hong Liang amenukuliwa leo na gazeti la Global New Light la Myanmar akiwaambia maafisa wakuu wa serikali kuwa "Msimamo wa China kuhusu mashambulizi ya kigaidi katika jimbo la Rakhine ni wazi, ni suala tu la ndani ya nchi" na hatua ya walinda usalama wa Myanmar dhidi ya magaidi wenye misimamo mikali pamoja na hatua za serikali kutoa misaada kwa watu zinaungwa mkono kikamilifu.
Suu Kyi anatarajiwa kuhutubia taifa siku ya Jumanne. Wakosoaji wametaka apokonywe tuzo la amani kwa kushindwa kumaliza machafuko ambayo pia yamehusisha uteketezaji wa vijiji na kusababisha Warohingya Waislamu 380,000 kukimbilia Bangladesh

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...