Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kim Jong-un: Jeshi letu lazima liwe sawa na la Marekani

MTEULE THE BEST
Rais Kim Jong un wa Korea kaskazini ameapa kwamba atahakikisha kuwa jeshi la taifa hilo lina uwezo sawa na ule wa MarekaniHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionRais Kim Jong un wa Korea kaskazini ameapa kwamba atahakikisha kuwa jeshi la taifa hilo lina uwezo sawa na ule wa Marekani
Korea Kaskazini imetangaza kuwa lengo lake kuu kijeshi kwa sasa ni kuhakikisha inakuwa na uwezo sawa na Marekani.
Shirika la habari la Korea Kaskazini lilitoa taarifa hiyo baada ya kombora la majaribio la mwisho kufanywa, ikisema kuwa kiongozi wa taifa hilo, Kim Jong-Un, amesema kuwa hataki kusikia Marekani ikisema itakabiliana na Korea Kaskazini kijeshi.
KIongozi wa taifa hilo Kim Jong un ameapa kuhakikisha kuwa taifa hilo linaafikia mpango wake wa kinyuklia kulingana na vyombo vya habari vya taifa hilo.
Lengo lake ni kuhakikisha jeshi la tifa hilo lina uwezo sawa na lile la Marekani kulingana na chom,bo cha habari cha KCNA kilichomnukuu kiongozi huyo.
Rais Kim Jong Un pamoja na maafisa wakuu wa jeshi wakisherehekea urushaji wa kombora jingineHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionRais Kim Jong Un pamoja na maafisa wakuu wa jeshi wakisherehekea urushaji wa kombora jingine
Matamshi ya bwana Kim yanajiri baada ya taifa hilo kufanyia majaribio kombora lake kupitia anga ya Japan, likitajwa kuwa kombora lililosafiri kwa umabli mkubwa zaidi
.Hatua hiyo imesbabishwa mgawanyiko miongoni mwa mataifa ambayo yaliunga nyuma ya uMoja wa Matifa dhidi ya Korea kaskazini siku chache zilizopita.
Lazima tuyaonyeshe mataifa yaneye uwezo mkubwa vile taifa letu litakavyokamilisha mpango wake wa kinyuklia licha ya vikwazo visivyoisha, bwana Kim alinukuliwa na chamobo cha habari cha KCNA
Alisema kuwa lengo la Korea Kaskazini ni kuwa na jeshi lenye uwezo sawa na lile la Marekani ili kuwazuia watawala wa marekani kutotaja swala la kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya Korea Kaskzini
Makombora ya Korea kaskazini yaliofanyiwa majaribio
Image captionMakombora ya Korea kaskazini yaliofanyiwa majaribio
Katika mkutano wa dharura, baraza la Usalama la umoja wa Mataifa, lilishutumu Korea Kaskazini kwa kufyatua Kombora juu ya Japan, lakini likasisitiza kuwa hakutakuwepo na vikwazo zaidi dhidi ya taifa hilo.
Awali Marekani ilionya kuwa Korea Kaskazini itashambuliwa kijeshi iwapo vikwazo ilivyowekewa havitatekeleza chochote.
Lakini Uchina kwa upande wake ilihimiza Marekani ikome kutoa vitisho na badala yake ianze kufanya mashauriano.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...