MTEULE THE BEST Haki miliki ya pichaAFPImage captionEneo ambalo kaburi la mwana wa Pharao lilipatikana
Kaburi la miaka 3,700 la mwana wa kike wa Pharaoh linaamika kupatikana karibu na mabaki ya piramidi iliogunduliwa Misri.
Wizara ya mambo ya kale imesema kuwa kaburi hilo lililopo katika eneo la kifalme la Dahshur Kusini mwa Cairo lilikuwa na sanduku la mbao lililochongwa.
Ndani ya sanduku hilo kulikuwa na mitungi iliojaa nguo za mapambo vikiwemo viungo vya marehemu ambaye ni mwana wa kike wa mfalme Emnikamaw.
Piramidi hiyo ya mfalme ina urefu wa mita 600 kutoka kwa kaburi hilo.
Mwezi uliopita watalam wa vitu vya kale wanaochunguza mabaki ya jengo hilo walipata afueni kwa kupata picha za mabaki hayo zilizokuwa na jina la Emnikamaw.
Pia waligundua mabaki ya makaburi ya mawe.
Haki miliki ya pichaNEVINE EL-AREF / EGYPTIAN MINISTRY OF ANTIQUITIESImage captionSanduku la vitu vya kulinda Viungo vya mwana wa Pharaoh
Dahshur ni eneo ambalo mfalme Sneferu wa awamu ya nne alijenga piramidi ya kwanza yenye urefu wa futi 341 iliokuwa na upande mmoja ambao ulikuwa umelainishwa takriban miaka 4000 iliopita.
Pia alijenga piramidi ya awali iliokuwa na urefu wa mita 105 ambayo mteremko wake ulikuwa na ngazi zilizobadilishwa kutoka pembe yenye digree 54 hadi 43.
Mfalme Sneferu alirithiwa na mwanawe Khufu anayejulikana sana kwa kujenga Piramidi kubwa katika eneo la Giza ambayo ilikuwa na urefu wa mita 138 ambayo ilikuwa maajabu ya dunia wakati huo.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.
Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...
Maoni