MTEULE THE BEST
Adrien Silva alitajwa kwenye benchi wakati wa mechi dhidi ya Huddersfield uwanjani King Power
Kiungo wa kati wa Ureno Adrien Silva hatimaye amefanikiwa kuhamia Leicester City, baada ya kushindwa majira ya joto klabu hiyo ilipochelewa kuwasilisha nyaraka zake kwa sekunde 14.
Fifa walikataa kuidhinisha uhamisho wa mchezaji huyo wa miaka 28 kutoka Sporting Lisbon wakati huo wakisema muda wa kuhama wachezaji ulikuwa tayari umepita.
Mreno huyo amekuwa akifanya mazoezi na Leicester kipindi chote cha majira ya joto kuimarisha kiwango chake cha uchezaji.
Uhamisho wake wa £22m ulikamilishwa Jumatatu na akatajwa kwenye benchi mechi ya Leicester nyumbani dhidi ya Huddersfield.
Silva, ambaye ni mzaliwa wa Ufaransa, alitoka akademi ya Sporting Lisbon, na amekuwa kwa mikopo Maccabi Haifa na Academica.
Adrien Silva amefunga bao moja katika mechi 20 alizochezea Ureno
Amechezea Ureno mechi 20 za kimataifa na kuwafungia bao moja na aliwachezea waliposhinda Euro 2016.
Silva amesema alipitia kipindi kigumu sana miezi hiyo minne akisubiri dirisha lifunguliwe tena Januari, lakini amekuwa akitia bidii kujiweka sawa kucheza.
Hayo yakijiri, Leicester wamemuita tena kiungo wao Harvey Barnes kutoka Barnsley alikokuwa kwa mkopo tangu Agosti
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni