Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Polisi yavunja maandamano ya Kanisa DR Congo

Watu wanane wameuawa Juampili na dazeni kadhaa kukamatwa na vikosi vya usalama katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, wakati wa maandamano yalioitishwa na Kanisa Katoliki kumshinikiza rais Joseph Kabila aachie madaraka




Licha ya maombi, hasa kutoka kwa Umoja wa Mataifa kuheshimu haki ya raia kuandamana, wanajeshi walifyatua hewa ya kutoa machozi ndani ya makanisa na risasi za moto hewani kuvunja mikusanyiko ya waumini wa Kikatoliki, na katika kisa kimoja waliwakamata wavulana wanaohudumu kanisani kwa kuongoza maandamano mjini Kinshasa.


Mawasiliano ya intanet yalikuwa chini mnamo wakati makundi ya Kanisa na kisiasa yakikaidi amri iliyowekwa na serikali na kuendelea na maandamano hayo. "Vifo nane -- saba mjini Kinshasa na kimoja Kananga," katikati mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, chanzo kutoka Umoja wa Mataifa kililiambiam shirika la habari la Ufaransa AFP, na kuongeza kuwa kulikuwepo na watu 82 waliokamatwa, wakiwemo mapadri, katika mji mkuu na 41 katika maeneo mengine ya nchi."

Kabila awaonya watakaofanya vurugu

Katika hotuba yake ya kumaliza mwaka, Kabila alisisitiza kuwa kutangazwa hivi karibuni kwa kalenda ya uchaguzi utakaofanyika Desemba 2018, "kunatupeleka pasina kurudi nyuma kuelekea kuandaliwa kwa uchaguzi".



Waandamanaji wakishinikiza rais Joseph Kabilaaachie madaraka mjini Kinshasa.

"Nawaalika mchukuwe jukumu (la mchakato wa uchaguzi) na mtekeleze haki yenu kupitia mchakato huu," aliongeza kusema katika hotuba hiyo iliyorekodiwa kabla na kutangazwa kupitia televisheni ya taifa.

Pia alionekana kutoa onyo kwa waandamanaji, akiwasihi raia kuchukuwa tahadhari ili "kuwazuwilia njia wale wanaotaka kutumia uchaguzi kama kisingizio katika miaka ya hivi karibuni, na ambao sasa wangejaribu kutumia vurugu, kuzuwia mchakato unaoendelea wa kidemokrasia kuitumbukiza nchi katika machafuko".

Msemaji wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Congo Florence Marchal alisema watu wasiopungua 82 wamekamatwa nchini kote kuhusiana na maandamano ya Jumapili. Alilaani matumizi ya nguvu dhidi ya maandamano ya amani na ukandamizaji wa haki.

Mkurugenzi wa shirika la kutetea haki za binadamu la Huma Rights Watch katika kanda ya Afrika ya Kati Ida Sawyer alisema vikosi vya usalama viliwapiga risasi na kuwauwa wanaume wawili nje ya Kanisa la Mt. Alphonse katika wilaya ya Matete.

Msemaji wa polisi ya Congo Kanali Pierrot Mwanamputu, hata hivyo, alisema wawili hao waliuawa baada ya kuzozana na polisi. Alisema askari wa polisi pia alifariki. Leonie Kandolo, msemaji wa mmoja ya makundi yalioandaa maandamano hayo, alisema zaidi ya watu 10 waliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa. Alisema pia kuwa wengine kadhaa, wakiwemo baadhi ya mapadri, wameweka kizuwizini.

Maandamano ya amani

Makanisa ya Kikatoliki na wanaharakati waliitisha maandamano ya amani baada ya ibada ya Jumapili, mwaka mmoja baada ya Kanisa Katoliki kusimamia utiaji saini wa makubaliano, yalioweka terehe mpya ya uchaguzi ili kupunguza mzozo katika taifa hilo lenye utajiri mkubwa wa madini.



Mkuu wa tume ya uchaguzi ya DR Cngo Corneille Nangaa.

Kabila ambaye muhula wake ulimalizika Desemba 2016, alikuwa amekubali kuitisha uchaguzi kufikia mwishoni mwa 2017. Tume ya Uchaguzi wa Congo inasema kura hiyo haiwezi kufanyika hadi Desemba 2018. Wakosoaji wanamtuhumu Kabila kwa kuahirisha uchaguzi ili kuendelea kusalia madarakani, na hivyo kusababisha wasiwasi kuongezeka na kuchochea vurugu na maandamano mabaya ya mitaani nchini kote tangu mwishoni mwa 2016.

Serikali ilikataa kutoa vibali kwa waandamaji siku ya Jumapili, na ilifunga mtandao wa intaneti na huduma za ujumbe mfupi nchini kote kabla ya maandamano hayo, kwa kile ilichosema ni sababu za kiuslama. Zaidi ya makanisa 160 yalishiriki katika maandamano hayo. Polisi ilijibu kwa kutumia gesi ya kutoa machozi katika baadhi ya maeneo ya mjini Kinshasa.

Tayari maandamano yalikuwa yametulia kufikia mchana, ingawa vizuwizi viliendelea kujengwa kuelekea sherehe za kuukaribisha mwaka mpya. Tume ya uchaguzi wa Congo imepanga tarehe mpya ya uchaguzi wa rais na bunge kuwa Desemba 23, 2018, ingawa upinzani umesema utakubaliana tu na ucheleweshwaji wa uchaguzi hadi Juni 2018.

Kabila anaweza kusalia madarakani hadi uchaguzi ujao utakapofanyika, ingawa anazuwiwa na katiba kuwania muhula mwingine. Taifa hilo halijawahi kuwa na makabidhiano ya amani ya madaraka tangu lilipopata uhuru wake kutoka kwa Ubelgiji mwaka 1960


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...