Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Liberia: George Weah amwalika Wenger sherehe ya kuapishwa kwake

MTEULE THE BEST

George Weah alikuwa mchezaji Monaco Wenger alipokuwa meneja

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ameambia BBC kwamba amepokea mwaliko kutoka kwa rais mteule wa Liberia George Weah kuhudhuria sherehe ya kuapishwa kwake baadaye mwezi huu.

Wenger amesema: "Nimealikwa na George kwa siku hiyo ambapo ataapishwa kuwa Rais."

Meneja huyo wa Arsenal alikuwa meneja wa Weah katika klabu ya Monaco inayocheza Ligi Kuu ya Ufaransa miaka ya 1990 na amesema hakuwahi kufikiria kwamba wakati mmoja mchezaji huyo angekuwa rais.

"Maisha ya jamaa huyu kwa kweli ni kama filamu. Ni ya kushangaza. Yanaweza kuunda filamu nzuri sana," amesema Wenger.

"Nakumbuka nilipomuona mara ya kwanza Monaco alipofika na alikuwa anaonekana kukanganyikiwa kidogo, hakuwa anamjua mtu yeyote, na hakuwa anatazamwa na wengi kama mchezaji stadi na baadaye akaibuka na kuwa mchezaji bora duniani 1995 na leo hii sasa amekuwa rais wan chi. Ni kisa cha kushangaza," Wenger ameongeza.


Wenger amesema Weah kwa muda mrefu amekuwa anaipenda sana nchi yake na ana ukakamavu ambao umemfanya kuamini kwamba alikuwa na ndoto fulani maishani.

"Nilisafiri na George wakati huo kulipokuwa na vita nchini Liberia na nimeona jinsi alivyotatizika kutokana na taifa lake na hilo lilikuwa jambo moja ambalo lilikuwa linaendelea kwa muda taifa lake, upendo wake kwa taifa hilo na watu wake," amesema Wenger.

"Leo hii nikitazama nyuma na kumuona akitokwa na machozi vita vilipokuwa vimechacha Liberia ni jambo la kufurahisha sana na natumai atakuwa rais wa furaha na ningependa kuona bwana huyu akiwa mfano mzuri kwa wachezaji wote wa soka wa sasa."

Wenger amesema kwamba hataweza kusafiri Liberia kuhudhuria sherehe hiyo ya kuapishwa kwa Weah kutokana na shughuli nyingi Ligi ya Premia.


Wenger alikuwa mkufunzi wa George Weah miaka ya 1990 Monaco

"Ninaamini nitakuwa na shughuli nyingi lakini iwapo nitapigwa marufuku basi nitapata muda wa kwenda," Wenger, ambaye amefunguliwa mashtaka ya utovu wa nidhamu na Chama cha Soka England amesema.


Weah alishinda duru ya pili ya uchaguzi mwezi jana dhidi ya aliyekuwa makamu wa rais Joseph Boakai kwa kupata zaidi ya 60% ya kura.

Atachukua nafasi ya Ellen Johnson Sirleaf rais wa kwanza mwanamke kuwahi kuchaguliwa kuongoza taifa la Afrika


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...