Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tanzania yafafanua madai ya upotevu wa trilioni 1.5

Baada ya juma zima la kuwepo kwa hofu ya kutoweka kiasi cha shilingi trilioni 1.5 za Kitanzania serikalini, hatimaye leo serikali ya Rais John Magufuli imetoa ufafanuzi bungeni juu ya wapi kilipo kiasi hicho cha fedha.



Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli.

Baada ya juma zima la kuwepo kwa hofu ya kutoweka kiasi cha shilingi trilioni 1.5 za Kitanzania katika mazingira ya kutatanisha katika makadirio ya bajeti ya serikali ya Tanzania, hatimaye leo serikali ya Rais John Magufuli imetoa ufafanuzi bungeni juu ya wapi kilipo kiasi hicho cha fedha.


Ufafanuzi huu unatolewa baada ya kuwepo kwa kile kilichoonekana kama ukosoaji wa wazi na wasiwasi juu ya matumizi mabaya ya fedha za umma na yasiozingatia sheria kutoka kwa viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani na hata wananchi wa kawaida kwa takribani juma zima.

Akitoa mchanganuo wake, Naibu Waziri huyo wa Fedha na Mipango Dk. Ashatu Kijaji amesema kiasi cha shilingi bilioni 697 kilitumika kwa matumizi ya dhamana na hati fungani zilizoiva. Na kingine bilioni 687 kilikuwa kwa ajili ya mapato tarajiwa.

Fungu la fedha kwa ajili ya Zanzibar

Rais John Magufuli na Rais wa Zanzibar Ali Mohammed Shein

Aidha naibu waziri aliongeza kusema kiasi shilingi bilioni 203 kilikusanywa kama kodi kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Amesema kutoonekana kwa fedha hizo kunatokana na taarifa ya ukaguzi wa Mkaguzi wa Mdhibiti wa Hesabu za Serikali CAG kutumia nyaraka za hesabu mbalimbali, na hivyo kutojumuisha taarifa za utekelezaji wa bajeti, akiongeza kuwa hadi Juni mwaka 2017 mapato yalifikia shilingi trilioni 25.3. na matumizi kufikia trilioni 23.79.

Ukosoaji wa serikali unaendelea

Hata hivyo, tayari ufafanuzi huu wa serikali juu ya zilipo shilingi trilioni 1.5 umeanza kukosolewa vikali. Msemaji wa chama cha upinzani cha ACT-Wazalendo, Ado Shaibu, ambaye chama chake ndicho kilichoanzisha udadisi wa matumizi ya fedha hizo, ameiambia DW kwa njia ya simu kuwa bado serikali haijasema ukweli na kwamba wanajiandaa kueleza upungufu uliojitokeza.

Itakumbukwa hivi karibuni nchini humo, baada ya taarifa ya mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali kuwekwa hadharani kiongozi wa  chama cha siasa cha upinzani cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, alijitokeza hadharani kusema fedha hizo hazikutolewa kwa matumizi kwa hivyo hazikukaguliwa, na hivyo kuzusha mjadala unaoendelea hadi wakati huu.

Sakata hili la shilingi trilioni 1.5 ni la kwanza la aina yake kwenye taifa hilo kubwa la Afrika Mashariki na wengi wanalichukulia kuwa ni suto kwa utawala wa miaka miwili wa Rais Magufuli, ambaye amejijengea sifa ya kupambana na ufisadi, ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za umma

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...