Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Malkia Elizabeth II wa Uingereza atimiza miaka 92

Malkia Elizabeth II 
Sherehe kubwa zinafanyika katika kasli la kifalme mjini London, Uingereza, kuadhimisha miaka 92 ya kuzaliwa Malkia wa nchi hiyo, Elizabeth II. Sharehe hizo zimekwenda sambamba na mkutano wa kilele wa Jumuiya ya Madola.


Malkia wa Uingereza, Elizabeth II amesherehekea miaka 92 ya kuzaliwa, katika sherehe iliyohudhuriwa na nyota kadhaa katika fani ya burudani. Mizinga ya kukokotwa na farasi imefyatuliwa mara 41 kwa heshima yake katika bustani ya Hyder Park na mara 61 kwenye mnara wa London. Kwenye Kasli la Windsor, kikosi cha ulinzi wa ufalme kimemwimbia Malkia Elizabeth II wimbo wa ''Happy Birthday'' wakati wa kubadilishana zamu.

Jioni ya leo Malkia na familia yake wanatarajia kutumbuizwa na wasanii kutoka nchi mbali mbali za Jumuiya ya Madola. Wakuu wa jumuiya hiyo yenye nchi 53 wanachama wamekuwa wakikutana mjini London katika mkutano wao wa kilele unaofanyika kila baada ya miaka miwili.
Wasanii watakaotumbuiza hafla hiyo  ni pamoja na Kylie kutoka Australia, Shawn Mendes kutoka Canada, bendi ya Ladysmith Black Mambazo ya Afrika Kusini, na nyota wa Reggae Mmarekani mwenye asili ya Jamaica, Shaggy. Kutoka Uingereza kwenyewe wasanii watakaoshiriki katika sherehe hiyo ni Tom Jones, Craig David na Sting.
Katika sherehe hizo zitakusanywa fedha zitakazowekwa katika fuko la hisani la Malkia Elizabeth, ambalo linasimamiwa na mjukuu wake, Mwanamfalme Harry ambaye pia anatarajiwa kutoa hotuba.
Malkia Elizabeth II amekuwa kama nembo ya Jumuiya ya Madola inayoishirikisha Uingereza na nchi zilizowahi kuwa makoloni yake, tangu kufariki kwa baba yake, Mfalme George VI mwaka 1952

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...