Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Man Utd ndiyo klabu yenye thamani kubwa zaidi Ulaya

Manchester United na Chelsea zote zimo kwenye 10 bora

Manchester United kwa mara nyingine wametangazwa kuwa klabu yenye thamani ya juu zaidi Ulaya, ambapo thamani yao inakadiriwa kuwa ā‚¬3.25bn (Ā£2.9bn) kwa mujibu wa kampuni ya KPMG.


Klabu hiyo ya England inaongoza kwa "thamani ya biashara", ikiwa mbele ya klabu nyingine kama vile Real Madrid na Barcelona.


Orodha hiyo imeandaliwa baada ya utafiti uliofanywa kwa kuangazia taarifa za kifedha za misimu ya 2015-16 na 2016-17 ambapo waliangazia faida, haki za utangazaji, umaarufu, matarajio kutokana na uwezo wa kimichezo na thamani ya uwanja.


Liverpool, ambao wamefika fainali Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya wamo nafasi ya nane kwenye orodha hiyo.


Kwenye utafiti huo ulioangazia klabu 32 kubwa, klabu za Ligi Kuu ya England zinajaza nafasi sita kati ya 10 za kwanza.


Andrea Sartori, mkuu wa michezo duniani katika KPMG ambaye ndiye mwandishi wa ripoti hiyo, anasema kwa jumla thamani ya klabu za soka imepanda katika mwaka uliopita.



"Ukuaji wa jumla unatokana na sababu kadha, moja ikiwa ni kuongezeka kwa mapato yanayotokana na uendeshaji shughuli katika klabu 32 kuu, ambao ulikuwa ni ukuaji 8%," alisema.


"Uhamisho wa wachezaji wa pesa nyingi pamoja na kuongezeka kwa mishahara hakujazuia klabu kuendelea kuongeza mapato, kwani faida kabla ya kutozwa ushuru uliongezeka kwa mara 17 ukilinganisha na mwaka uliotangulia."


Klabu 10 bora Ulaya kwa 'thamani ya biashara'


Manchester United - ā‚¬3.255bn


Real Madrid - ā‚¬2.92bn


Barcelona - ā‚¬2.78bn


Bayern Munich - ā‚¬2.55bn


Manchester City - ā‚¬2.16bn


Arsenal - ā‚¬2.10bn


Chelsea - ā‚¬1.76bn


Liverpool - ā‚¬1.58bn


Juventus - ā‚¬1.30bn


Tottenham - ā‚¬1.29bn


Chanzo: KPMG


Kando na kutawala orodha ya 10 bora, kulikuwa na klabu nyingine tatu za Uingereza katika orodha ya 20 bora - West Ham United, Leicester City na Everton.


SSC Napoli (nafasi ya 17) nao wamekuwa klabu ya pili kwa thamani Italia, nyuma ya Juventus lakini mbele ya AC na Inter Milan.


Mwaka huu, klabu 12 zilikuwa na thamani ya zaidi ya euro bilioni moja, mbili zaidi ya 2017 ambapo zilikuwaklabu kumi pekee.




Na klabu sita zina thamani ya zaidi ya euro bilioni mbili, tatu kutoka Ligi ya Premia, mbili kutoka Uhispania na moja ya Ujerumani.


Misimu ya 2015-16 na 2016-17, Manchester United walishinda Kombe la FA, Kombe la Ligi na Europa League. Lakini msimu huu wamemaliza bila kikombe hata kimoja


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...