Ruka hadi kwenye maudhui makuu

UEFA Ligi ya Mabingwa Ulaya Champions League: Nani atawika fainali Kiev kati ya Salah, Ronaldo na Milner?


Mohamed Salah, Cristiano Ronaldo na James Milner

Fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya Jumamosi itakuwa kati ya timu ambazo zimefunga mabao mengi zaidi msimu huu huku washambuliaji bora zaidi duniani wakikutana.


Real Madrid wanatafuta ushindi wa 13 na wa tatu mfulizo huku Liverpool wakiweza kupanda juu ya Bayern Munich na Barcelona nyuma na AC Milan katika orodha ya vilabu vilivyopata ushindi mara nyingi zaidi katika European Cup na Champions League ikiwa wataibuka washindi huko Kiev.


Milner anaweza kuwa na umuhimu usiotarajiwa Kiev?


Zikiwa zimefunga zaidi ya mabao 90 kwenye mashindano yote msimu huu ni wazi kuwa fainali hii itakuwa kama vita kati ya Cristiano Ronaldo wa Real Madrid na Mohamed Salah wa Liverpool.


Wote wako mbioni kun'gang'ania tuzo ya Ballon d'Or mwishoni mwaka 2018, lakini pia kuna mwanamume ambaye bila kutarajiwa huenda akawa mwenye umuhimu mkubwa huko Kiev.


James Milner alionyesha ubabe wakati wa nusu fainali dhidi ya Roma wakati alifikisha mchango wake muhimu katika mechi hadi mara 8 msimu huu na kusawazisha rekodi iliyowekwa na Neymar mwaka 2016-17.




Ni nani anakumbwa na harakati zaidi katika safu ya ulinzi?


Wakati wa kuanza kwa msimu kulikuwa na shaka kuhusu safu ya ulinzi ya Liverpool, lakini kufuatia kuwasili kwa Virgil van Dijk mwezi Januari na kuimarika kwa kipa Loris Karius inamaanisha kuwa tena hakuna udhaifu.


Kwa Real ni kitu tofauti.



Walikosa mchango wake Sergio Ramos wakati wa duru ya pili ya mechi kati yao na Juventus.


Liverpool nao wana matatizo yao, wameshindwa mara 13 kwenye Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya ikiwemo mara sita dhidi ya Roma na sare yao ya mwisho.


Lakini kikosi hicho cha Jurgen Klopp kimeshinda mara sita mfululizo msimu huu rekodi iliyowekwa na Barcelona.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...