Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Trump asema Korea Kaskazini imetoa majibu ya "ukarimu", "ufanisi"




Rais Donald Trump

Rais Donald Trump amesema Ijumaa asubuhi kuwa Korea Kaskazini imetoa mrejesho wa ā€œukarimuā€ na ā€œufanisi" baada ya kusitisha mkutano wake na Kim Jong Un.


ā€œNi habari nzuri sana kupokea kauli ya mrejesho ya upole na ufanisi kutoka Korea Kaskazini,ā€ Trump amesema katika ujumbe wa Twitter Ijumaa asubuhi.

ā€œHivi karibuni tutafahamu kile kitakachoendelea, ni matumaini yangu itakuwa ni utajiri na amani ya kudumu na ya muda mrefu. Ni wakati peke yake (na kipaji) utatuthibitishia hili.

Korea Kaskazini imesema Ijumaa bado iko tayari kufanya mazungumzo na Marekaniā€ wakati wowote, [katika] mpangilio wowote.ā€

Makamu Waziri wa Mambo ya Nje Kim Kye Gwan, mwakilishi katika mazungumzo ya nyuklia wa muda mrefu na mwanadiplomasia wa ngazi ya juu, amesema katika tamko lililotangazwa na shirika la habari la serikali la Korea Kaskazini iko ā€œtayari kuipa Marekani muda na fursaā€ kufikiria suala la mazungumzo.

Trump alijitoa kufanya mkutano na Kim kama ilivyokuwa imepangwa Alhamisi asubuhi, akilaumu matamko yaliyotolewa na Pyongyang hivi karibuni yakitishia kutoshiriki katika mkutano huo kwa kile waliocho kiona ni kauli za mashambulizi ziliotolewa na maafisa wa Marekani

Mwanadiplomasia wa Korea Kaskazini amesema kauli kali za Pyongyang zilisababishwa na kujigamba kwa Marekani kulikopita kiasi, na uhasama uliojitokeza hivi sasa unaonyesha ā€œumuhimu mkubwaā€ wa kuwepo mazungumzo hayo.

ā€œJapokuwa tuko kimya tunaridhishwa na uamuzi wa kishujaa wa Rais Trump ambao hakuna rais yoyote wa Marekani aliwahi kujaribu kuchukua, na kufanya juhudi kuandaa tukio hilo muhimu la mkutano huo,ā€ tamko la Kim Kye Gwan limesema

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...