Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kikosi cha Kenya cha Olimpiki chatajwa

MTEULE THE BEST

 



Kamati ya olimpiki nchini Kenya, Nock, na shirikisho la riadha nchini Kenya, AK, zimetaja timu itakayoiwakilisha Kenya mjini Rio, nchini Brazil Agosti mwaka huu.
Ingawa wanariadha wawili wa kwanza katika kila kitengo walijanyakulia tiketi, Kikosi cha Kenya pia kimeangazia masuala mengine kama vile fomu ya wanariadha, matokeo yao katika mbio za riadha duniani yakiwemo mashindano ya hivi karibuni ya riadha nchini Afrika Kusini.
Mwanariadha anayeshikilia rekodi ya Olimpiki katika mbio za mita mia nane, David Rudisha, amepewa fursa nyingine ya kushiriki katika Olimpiki licha ya kubwagwa na Alfred Kipketer.
 
Yego
Licha ya kujiondoa kutoka mbio za mita elfu kumi, bingwa wa Dunia, Geodfrey Kamworor ni miongoni mwa wanariadha watakaowania medali katika mbio hizo ifikapo Agosti. Kamworor, na Bedan Karoki wataungana na mshindi wa mbio za majaribio Paul Tanui, na mwenzake Charles Yosei aliyenyakua nafasi ya pili.
"Ninafuraha kubwa kuiwakilisha Kenya Katika Olimpiki. Natarajia nitafanya vyema katika mashindano ya Olimpiki," alisema Tanui.
Katika mbio za mita mia nane, upande wa kina dada, mshindi wa mbio za majaribio Margaret Nyairera Wambui, anatarajia ushindani mkali kutoka Eunice Sum, na Winnie Chebet wakati watakapokutana kwenye olimpiki licha ya kuwabwaga katika mbio za majaribio.
 
Vivian Cheruiyot
Hata hivyo Kenya inatarajia ushindani mkali kutoka kwa Caster Semenya.
"Ni majivuno makubwa kufuzu na naamini hakuna mtu asiyeweza kushindwa, nia yangu ni kuondoka na dhahabu, alisema mshindi wa mbio za majaribio, Margaret Nyairera.''
Kwa upande wa mbio za mita mia nne kuruka vihunzi, bingwa wa dunia Nicholas Bett na pacha wake, Aaron Koech waliitwa kwenye timu hiyo. Kujumuishwa kwa Bett kuliwashangaza wengi kwani hakushiriki kwenye majaribio.
Bingwa wa mbio za mita elfu tano na elfu kumi upande wa wanawake, Vivian Cheruiyot, alitajwa katika timu zote mbili ambapo analenga kuwania katika vitengo vyote viwili.
Wengine waliotajwa ni mrusha mkuki, Julius Yego, ambaye atakuwa mwakilishi pekee wa Kenya katika mashindano ya Rio.
''Tunawapongeza wote waliofuzu, na wakati huu tunatarajia kujiandaa ipasavyo ili kufanya vyema katika mashindano ya Rio," alisema rais wa riadha nchini Kenya, Jackson Tuwei.
ORODHA KAMILI - WANAUME 200m: Kevin Nkanata, Mike Mokamba 400m Hurdles: Nicholas Bett, Boniface Mucheru, Aron Koech 400m: Alphas Kishoyan, Raymond Kibet, Alex Sampao, Boniface Mweresa 800m: Alfred Kipketer, Ferguson Rotich, David Rudisha 1500m: Asbel Kiprop, Elijah Manangoi, Ronald Kwemoi 3000m S/Chase: Brimin Kipruto, Conceslus Kipruto, Ezekiel Kemboi 5000m: Caleb Mwangangi Ndiku, Isaiah Kiplangat Koech 10000m: Paul Tanui, Charles Yosei, Geoffrey Kamworor, Bedan Karoki Marathon: Eliud Kipchoge, Stanley Biwott, Wesley Korir Kurusha mkuki: Julius Yego Kutembea 20km: Samuel Gathimba, Simon Wachira High Jump: Mathew Sawe
ORODHA KAMILI WANAWAKE 400m Hurdles: Maureen Jelagat 400m: Maureen Jelagat, Margaret Nyairera Wambui 800m: Margaret Nyairera Wambui, Eunice Sum, Winnie Chebet, 1500m: Faith Chepngetich, Nancy Chepkwemoi. Viola Lagat 3000m S/Chase: Hyvin Kiyeng, Beatrice Chepkoech, Lydia Rotich 5000m: Vivian Cheruiyot, Hellen Obiri, Mercy Cherono 10000m: Vivian Cheruiyot, Betsy saina, Alice Aprot Marathon:Jemima Sumgong, Helah Kiprop, Visline Jepkesho Kutembea 20km: Grace Wanjiru

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...