Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KRISTO NA KAZI YAKE

MTEULE THE BEST

 TUMSIFU YESU KRISTO WAPEDWA KATIKA KRISTO!!!

MADA YA LEO : KRISTO NA KAZI YAKE

SOMO:WAKOLOSAI 1:15-23


 

Kristo ni mfano wa MUNGU asiyeonekana; ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.

Maana kwake viumbe vyote viliumbwa kila kitu duniani na mbinguni vitu vinavyoonekana na visivyoonekana: wenye enzi, watawala,wakuu na wenye nguvu  Vyote viliumbwa kwake na kwa ajili yake.

Yeye alikuwako kabla ya vitu vyote ; vyote uendelea kuwako kwa uwezo wake.

Yeye ni kichwa cha mwili wake, yaani kanisa; yeye nichanzo cha uhai yaani huo mwili.

Yeye ndiyo mwanzo , mzaliwa wa kwanza aliyefufuliwa kutoka wafu ili awe na nasfi ya kwanza katika vitu vyote.

Maana MUNGU aliupenda utimilifu wake woteuwe ndani yake.

Kwake vitu vyote vilipatanishwa na MUNGU: na kwa damu yake msalabani akafanya amanina vitu vyote duniani na mbinguni.

Hapo kwanza nyinyi pia mlikuwa mbali  na MUNGU na mlikuwa adui zake kwa sababu ya fikra zenu na matendo yenu maovu.

Lakini sasa, kwa kifo cha mwanae aliyeishi hapa duniani , MUNGU amewapatanisha naye, kusudi awaweke mbele yake mkiwa watakatifu , safi na bila lawama  

Mnapashwa lakini kuendelea na msingi imara katika imani  wala msikubali kutikishwa kutoka katika tumaini lile mlilopata wakati mlipo sikia injili  mimi PAULO nimekuwa mtumishi  wa hiyo injili ambayo imekwishaubiliwa na kila mtu duniani 

NENO LA BWANA............

Tumuombe Mungu atuongoze katika njia ya kweli na haki daima na milele

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...