Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Antonio Guterres kuwa Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa

MTEULE THE BEST

Antonio Guterres (picture-alliance/dpa/J.-Ch. Bott)
Waziri mkuu wa zamani wa Ureno Antonio Guterres anatarajiwa kutangazwa rasmi kuwa Katibu mkuu mpya wa Umoja wa Mataifa baada ya kupigiwa kura nyingi kuliko wagombea wengine katika baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Baada ya duru ya sita ya kura isiyo rasmi katika baraza la usalama la Umoja wa Mataifa siku ya Jumatano, Antonio Guterres anatarajiwa kutangazwa rasmi Alhamisi kuwa Katibu mkuu mpya wa Umoja wa Mataifa.
Guterres ambaye alikuwa mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu wakimbizi UNHCR kwa miaka kumi iliyopita, alipata kura 13 kati ya 15 za nchi wanachama wa baraza hilo la usalama huku nchi zote tano wanchama wa kudumu walio na kura ya turufu wakimuunga mkono.
Balozi wa Urusi katika Umoja wa Mataifa Vitaly Churkin alitangaza kuwa ni bayana kuwa Guterres ndiye atachukua wadhifa unaoshilikiwa na Ban Ki Moon mwenye umri wa miaka 72, waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Korea Kusini ambaye anakamilisha mihula yake miwili ya miaka kumi katika wadhifa huo.
Kura ya mwisho ya kumuidhinisha katibu mkuu mpya wa Umoja wa Mataifa itapigwa hii leo. Guterres mwenye umri wa miaka 67 ameahidi kuuboresha Umoja wa Mataifa, kuimarisha juhudi za kulinda amani na kulinda haki za binadamu.
European Parliament in Strasbourg Ban Ki Moon (picture-alliance/dpa/P. Seeger)
Katibu mkuu wa sasa wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon
Guterres ambaye alikuwa waziri mkuu wa Ureno kuanzia mwaka 1995 hadi 2002, amekuwa akiongoza katika kura zisizo rasmi za kumchagua katibu mkuu mpya tangu Julai lakini uamuzi wa jana wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa karibu kwa kauli moja kumchagua mwanasiasa huyo wa kisosholisti haukutarajiwa.
Atakuwa kiongozi wa kwanza wa nchi kuwa mkuu wa Umoja wa Mataifa, wadhifa ambao umeshikiliwa na mawaziri kadhaa wa mambo ya nje ambao walikuwa wakichaguliwa katika vikao vya faragha vya Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa. Kipindi hiki; zoezi hilo liliendeshwa kwa uwazi zaidi na wagombea waliruhusiwa kuhudhuria vikao ili kujinadi mbele ya mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Akishaidhinishwa na baraza la usalama, Guterres atawasilishwa kwa mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa ili kuidhinishwa rasmi kuwa katibu mkuu wa tisa wa Umoja huo. Katibu mkuu mpya ataanza kutekeleza majukumu yake tarehe 1 Januari kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
USA Antonio Guterres in New York (Getty Images/AFP/K. Betancur)
Katibu mkuu mtarajiwa wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres
Balozi wa Ufaransa Francois Delatter amesema kumchagua Guterres anayezungumza kiingereza, kifaransa, kihispani na kireno ni habari njema kwa Umoja wa Matifa huku balozi wa Uingereza Matthew Rycroft akisema atakauwa katibu mkuu shupavu.
Katika kinyang'anyiro hicho cha kumchagua katibu mkuu mpya wa Umoja wa Mataifa kumekuwa na wito wa kuchaguliwa kwa mara ya kwanza mwanamke. Kulikuwa na wanawake saba waliogombea wadhifa huo. Pia kulikuwa na wito wa kuchaguliwa mtu kutoka Ulaya mashariki, eneo ambalo mpaka sasa halijawakilishwa katika wadhifa huo kwa miaka 70 iliyopita.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...