Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Udhibiti wa mipaka waanza Ulaya

MTEULE THE BEST


Bulgarien TĆ¼rkei Grenze - Start von Frontex Grenz- und KĆ¼stenschutzagentur (Getty Images/AFP/D. Dilkoff)Shirika jipya la kudhibiti mipaka na pwani la Umoja wa Ulaya limeanza shughuli zake katika mpaka baina ya Bulgaria na Uturuki, huku Umoja huo ukitarajia hatua hiyo itamaliza mzozo miongoni mwa wanachama.
Maafisa wa Umoja wa Ulaya wamezindua mpango huo leo katika kivuko cha mpaka wa Andreevo ulioko baina ya Uturuki na Bulgaria ambao wahamijai wengi huutumia ili kuingia katika bara la Ulaya.  Lengo la kuanzishwa kwa kikosi hicho cha kudhibiti mipaka katika Umoja wa Ulaya ni kutafuta mfumo sawia utakao tumiwa kupambana na swala la uhamiaji haramu.
Waziri wa mambo ya ndani wa Bulgaria  Rumyana Bachvarova  amesema kuwa uzinduzi huo wa leo ni jambo  muhimu kwa bara zima la Ulaya kuweza kutokea. Pia ameeleza kwamba kuzinduliwa kwa shirika hilo jipya ni mwanzo wa ushirikiano mzuri na hatua zitakazoleta mafanikio katika mipaka ya Ulaya.
"Kuilinda mipaka yenye uhakika ndio jukumu letu kubwa hasa katika wakati huu wa mgogoro wa wakimbizi. Ili kufanikisha zoezi hili, tunahitaji kugawana majukumu na pia kufanya kazi kwa pamoja, sisi kama wanachama wa Umoja wa Ulaya vile vile kwa mashirika yetu. Nina uhakika kwamba kuanzia leo shirika hili jipya la kudhibiti mipaka na pwani litaboresha shughuli zinazohusiana na mipaka ya nchi kavu, angani na majini katika hatua ambazo zitaleta usalama kwa kiwango cha juu katika Umoja wa Ulaya."   
Griechenland Lesbos RĆ¼ckfĆ¼hrung von FlĆ¼chtlingen in die TĆ¼rkei (Reuters/G. Moutafis)
Wakimbizi katika mpaka wa Uturuki na Ugiriki wakidhibitiwa na walinzi wa mpakani, Frontex.
Wakati huo huo kamishna wa Umoja wa Ulaya Dimitris Avramopoulos ameisifu hatua hiyo kuwa ni hatua mojawapo ya maendeleo katika historia ya kudhibiti mipaka barani Ulaya wakati alipozungumza na waandishi wa habari leo hii.
"Shirika la kudhibiti mipaka na pwani limekuwa sasa ni jambo la kweli hili limewezekana katika kipindi cha chini ya miezi tisa tangu Kamisheni ya Umoja wa Ulaya ilipolipendekeza.  Wananchi wa Ulaya wametaka na wana haki ya kupata majibu ambayo leo hii tumeyatoa majibu hayo kwa pamoja."

Kamishna huyo aliongezea kusema kuwa Shirika hilo jipya la kudhibiti mipaka na pwani la Umoja wa Ulaya limejengwa katika misingi ya ushirikiano na kugawana majukumu ya kulinda hata mipaka ya nje ya Umoja huo ni sawa na kusema mipaka ya nje ya nchi moja mwanachama  ni jukumu la nchi nyingine wanachama.
Kansela Angela Merkel amezungumzia jinsi Ujerumani inavyokemewa na nchi za Ulaya ya Kati na ya Mashariki kutokana na sera zake za mlango wazi kwa wahamiaji, sera ambazo wanadai kuwa zimewarahisishia wanaharakati wa kutoka kwenye makundi ya Kiislamu yenye misimamo mikali kuweza kuingia katika nchi za Ulaya na kufanya mashambulio ya kigaidi. Wahalifu hao huingia Ulaya kwa kusingizia kuwa ni wakimbizi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...