Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ethiopia yazindua reli ya umeme ya kipekee Afrika

MTEULE THE BEST

Reli mpya Ethiopia

Image captionReli hiyo imegharimu dola 4 bilioni za Marekani
Ethiopia na Djibouti zimezindua reli ya kisasa ya treni za kutumia nguvu za umeme ambayo inaunganisha mji mkuu wa Addis Ababa na mji wa bandarini wa Djibouti.
Reli hiyo imejengwa na kampuni mbili za Uchina, kwa gharama ya takriban dola 4 bilioni za Kimarekani ambazo zilitolewa na serikali ya Uchina kama mkopo.
Reli hiyo inatarajiwa kuipa Ethiopia njia rahisi ya kufikisha bidhaa zake, hasa mazao ya kilimo, hadi dandarini.
Uchumi wa Ethiopia umekuwa ukikua kwa kasi kutokana na ongezeko la uzalishaj wa kilimo na ukuaji pia wa miji.
Kwa mujibu wa Benki ya Dunia, Ethiopia, yenye watu 97 milioni ni moja ya mataifa yenye uchumi unaokua kwa kasi zaidi duniani kwa sasa.
Kwa mujibu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, uchumi wa taifa hilo ulikua kwa asilimia 10.2 mwaka 2014/15, na kasi hiyo inatarajiwa kuendelea mwaka 2016 na mwaka 2017.
Reli hiyo ni ya umbali wakilomita 752, na kasi yake ya wastani itakuwa kilomita 120 kwa saa, jambo litakalofupisha safari ya kutoka Addis Ababa hadi Djibouti kuwa chini ya saa kumi ikilinganishwa na siku mbili zilizotumiwa awali.
Reli hiyo ndio mradi wa pili mkubwa wa reli inayounganisha mataifa zaidi ya mawili ambayo imejengwa na kampuni za Kichina barani Afrika.
EthiopiaImage copyrightGETTY IMAGES
Image captionEthiopia inataka kujenga reli ya kisasa ya umbali wa 5,000km
Mradi huo mwingine ni reli ya Tazara inayounganisha jiji la Dar es Salaam, Tanzania na mji wa Kapiri Mposhi nchini Zambia.
Wakati wa ziara yake Ethiopia Mei 2013, naibu waziri mkuu wa China Wang Yang alisema mradi huo wa reli wa Ethiopia-Djibouti ni "Tazara ya enzi mpya."
Kinyume na mradi wa Tazara, ambao ulijengwa miaka ya 1970 kama mradi wa msaada wa kimataifa kutoka kwa serikali ya Uchina, reli hiyo ya Ethiopia-Djibouti ni mradi wa kibiashara kati ya kampuni za Kichina na serikali za mataifa hayo mawili ya Afrika.
Reli hiyo itaunganisha Addis Ababa na jiji la DjiboutiImage copyrightSHIRIKA LA RELI LA ETHIOPIA
Image captionReli hiyo itaunganisha Addis Ababa na jiji la Djibouti



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...