Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Uchaguzi Marekani: Pence na Kaine walumbana kuhusu Trump

MTEULE THE BEST

Pence na Kaine


Mgombea urais mwenza wa chama cha Republican nchini Marekani Mike Pence na mwenzake wa Democratic Tim Kaine wamelumbana kuhusu taarifa za kodi za Donald Trump kwenye mdahalo wa runinga..
Image copyrightREUTERS
Image captMgombea urais mwenza wa chama cha Republican nchini Marekani Mike Pence na mwenzake wa Democratic Tim Kaine wamelumbana kuhusu taarifa za kodi za Donald Trump kwenye

Bw Pence, ambaye ni gavana wa Indiana, amesema mgombea urais wa chama cha Republican Bw Trump alitumia "werevu" katika kutumia sheria za kodi kukwepa kulipa kodi.
Lakini Bw Kaine, seneta wa Virginia, alipinga wazo hilo la "werevu" akishangaa iwapo ilikuwa busara kukwepa kulipa pesa za kutumiwa kulipa wanajeshi au kufadhili elimu shuleni.
Bw Trump ameshutumiwa sana kutokana na rekodi yake ya ulipaji kodi.
Amekataa kufichua taarifa zake za ulipaji kodi lakini gazeti la New York Times majuzi lilifichua kwamba huenda amekwepa kulipa kodi kwa miaka 18 iliyopita.
Hili liliwezekana kwa sababu bw Trump, aliyewekeza katika biashara ya ujenzi na uuzaji wa hoteli, alipata hasara kubwa ya zaidi ya $900 milioni mwaka 1995.
Hajakanusha habari hizo.
Akimshambulia Bw Trump, Bw Kaine alisema: "Nafikiri sote tunaofanya hivyo [kulipa kodi] ni wajinga?"
Mike Pence na Tim KaineImage copyrightJOE RAEDLE
Image captionElaine Quijano amekuwa Mmarekani wa kwanza wa asili ya Asia kusimamia mdahalo wa kitaifa
Kaine, 57, alianzisha mjadala huo wenye hisia kali katika chuo kikuu cha Longwood, Virginia kwa kushangaa ni vipi Bw Pence angemtetea Donald Trump.
Lakini mpinzani wake wa Republican alimjibu kwa kumkosoa Hillary Clinton kwa kutumia barua pepe yake ya kibinafsi kwa shughuli rasmi pamoja na sera yake ya mambo ya nje ambayo alisema imesababisha vurugu katika baadhi ya maeneo duniani.

Mambo mengine makuu:

  • Bw Kaine alitaja makundi ya watu ambao Bw Trump amewatusi, wakiwemo wanawake na wanajeshi waliotekwa vitani
  • Akimjibu Bw Pence amesema Donald Trump amewatusi Wamarekani wachache ikilinganishwa na Bi Clinton
  • Kutumiwa kwa jamii katika shughuli za polisi ndiyo njia muhimu ya kupunguza uhasama baina ya polisi na Wamarekani Weusi, amesema Bw Kaine.
  • Lakini Bw Pence amemtuhumu Bi Clinton kwa kuwafanya polisi waonekane wabaya na kuwatuhumu kuwa wabaguzi wa rangi
  • Wazo la kwamba Donald Trump anaweza kuwa amiri jeshi mkuu "linatutia wasiwasi sana", amesema Bw Kaine
  • Pence amesema yeye na Bw Trump watapunguza kodi inayolipwa lakini bado waweze kulipia huduma za kijamii na afya
Sehemu kubwa ya mjadala iliangazia sera ya mambo ya nje.
Bw Pence amesema "Marekani si salama sasa" kuliko ilivyokuwa Rais Obama alipochaguliwa na akasema Bi Clinton anafaa kulaumiwa kutokana na kuchipuka kwa kundi la Islamic State.
Amesema Rais wa Urusi Vladimir Putin anaweza kumheshimu Trump kwa sababu ya nguvu zake, na mgombea wake. "Hilo ni wazi".
Lakini Bw Trump amewasifu pia viongozi wa kiimla, amesema Bw Kaine, na watu anaowaenzi ni Bw Putin, kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un na kiongozi wa zamani wa Libya Muammar Gaddafi.
Mdahalo huo ulisimamiwa na mtangazaji wa CBS News Elaine Quijano.
handshake
Umeandaliwa baada ya mdahalo wa wagombea urais uliofanyika wiki iliyopita, ambao ulifuatiliwa na watu 84 milioni kwa mujibu wa Nielsen.



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...