Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Donald Trump. Mkanda watolewa wakati mbaya

MTEULE THE BEST

USA Donald Trump entschuldigt sich fĆ¼r sexistische Aussagen (REUTERS)
Trump aliomba radhi Jumamosi (08.10.2016) kwa kutumia lugha hiyo chafu kuhusu kuwatomasa na kuwabusu wanawake katika mkanda wa video wa mwaka 2005.Kutolewa kwa mkanda huo kumeitibuwa kampeni yake na kusababisha kulaaniwa na wanachama wenzake kutoka chama chake mwenyewe cha kisiasa.
Trump amesema katika taarifa ya video iliowekwa kwenye mtandao wa Twitter "Nimefanya mambo ninayoyajutia.Mtu yoyote anayenifahamu anajuwa kwamba maneno haya hayamaanishi mim ni mtu wa aina gani.
Nimesema nilikuwa sio sahihi na naomba radhi."
Wanachama wenzake wa chama cha Republikan wamelaani lugha aliyoitumia mgombea huyo.Spika wa Baraza la Wawakilishi Paul Ryan afisa mwandamizi wa chama hicho amesema "amechafuliwa " na matamshi hayo na amefuta tukio la kampeni lililokuwa lifanyike Wisconsin pamoja na Trump hapo Jumamosi.
Wanachama wenzake wamuacha mkono
USA Sprecher des ReprƤsentantenhauses Paul Ryan (Getty Images/AFP/N. Kamm)
Spika wa Baraza la Wawakilishi la bunge la Marekani Paul Ryan.
Reince Preibus mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Chama cha Republikan amesema "Mwanamke yoyote hapaswi aelezewe kwa maneno hayo au kuzungumziwa kwa njia hiyo. Kamwe!"
Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi wa chama cha Republikan Jason Chaffetz wa Utah ambaye ni mmojawapo wa mkosoaji mkubwa wa Clinton amesema ametenguwa kumuidhinisha Trump akikiambia kituo cha televisheni cha CNN kwamba angelishindwa kumuangalia usoni mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka 15.
Mbunge wa Republikan Mike Coffman kutoka Colorado amekiambia kituo cha televisheni cha CBS kwamba Trump anapaswa akae kando na kwamba kushindwa kwake kufikia hatua hii inaonekana kuwa ni  jambo la uhakika.
Kauli hiyo imepelekea kuomba radhi hadharani kwa mara ya kwanza na Trump katika kampeni yake ya kuwania urais iliojaa matusi na kauli za kiburi.Katika ukanda huo wa video wa mwaka 2005 tajiri huyo aliyekuja kwa nyota wa vipindi vya televisheni alisikika akitumia lugha ya kudunisha wakati akimtongoza mwanamke aliyeolewa na kutomasa wanawake.
Amesema"Wakati unapokuwa nyota wanakuachia ufanye hayo.Unaweza kufanya chochote kile."
Mkanda watolewa wakati mbaya
USA Republikaner Wahlkampf Donald Trump in Reno, Nevada (Reuters/M. Segar)
Donald Trump.
Mkanda huo wa video ulirekodiwa na kipindi cha televisheni cha "Accesss Hollyood " wakati akiwa safarini ndani ya basi kwenda kurekodi sehemu ya igizo la "Days of Our Lives".
Mkanda huo wa video umetolewa ikiwa imebakia siku moja kabla ya kufanyika kwa madahalo wa pili baina ya wagombea urais Trump na Hilary Clinton hapo Jumapili usiku(09.10.2016) ambao unaonekana ni muhimu kwa Trump kujaribu kurudi tena kwenye umashuhuri baada ya uchunguzi wa maoni kuonyesha amefanya vibaya katika madahalo wa kwanza.
Amesema jambo hilo ni kutaka kuleta ubabaifu ili watu wasizingatie yale muhimu inayoyakabili Marekani leo hii.Amesema ataufunga mjadala wake wa kuwania urais kwa hoja kwamba mpinzani wake Clinton amefanya dhambi kubwa dhidi ya wanawake na pia kugusia uzinzi wa mume wake rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton.
Amesema watayajadili hayo zaidi siku zinazokuja.Wakutane naye hapo Jumapili.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...