Mashabiki wa Ubelgiji na Manchester United jana walijawa na furaha baada ya kusikia kwamba mshambuliaji wao Romelu Lukaku amevunja rekodi ya ufungaji katika timu yao ya taifa.
Romelu Lukaku alitajwa kuvunja rekodi hiyo kwa kuwapita Bernard Voorhoof na Paul Van Himst ambao wana mabao 30 huku goli dhidi ya Japan likimfanya yeye kufikisha 31 idadi ambayo hata Lukaku mwenyewe alijinasibu kuifikia.
Lakini sasa shirikisho la soka duniani FIFA limeibuka na kutoitambua rekodi hiyo ya Romelu Lukaku kwa kusema kwamba moja kati ya michezo ambayo Lukaku alifunga hautambuliki na shirikisho hilo.
Mechi hiyo ilikuwa mwaka 2014 ambapo Ubelgiji walicheza dhidi ya timu ya taifa ya Luxembourg ambapo Ubelgiji waliibuka kidedea kwa mabao 5 huku Romelu Lukaku akifunga mabao 3 kati ya hayo 5.
Kinachowafanya FIFA kuundoa mchezo huo kwenye rekodi zao ni kitendo cha Ubelgiji kufanya sub 7 badala ya 6 katika mchezo huo suala ambalo lilikuwa kinyume na sheria katika mechi hiyo.
Hii sasa inamaanisha Lukaku ana mabao 28 tu na kama anahitaji kuwa mfungaji bora wa muda wote nchini Ubelgiji itambidi kufunga mabo matatu ili kufikisha 31.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni