Mshambuliaji wa Manchester United Romelo Lukaku amesema amezaliwa kufunga na anaamini ataendelea kufanya hivyo pamoja na kuvunja rekodi ufungaji bora nchini Ubelgiji kabla ya mwaka huu kuisha.
Lukaku ameyasema hayo baada ya kuifikia rekodi ya Paul Van Himst na Bernard Voorhoof ya mabao 30 katika timu ya taifa ya Ubelgiji, ambapo ameeleza kuwa bado ana nia ya kufunga zaidi.
āNimezaliwa kwa ajili ya hili na nitaendelea kufanya hivyo", amesema Lukaku ambaye sasa anahitaji bao moja tu kuweza kuweka rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wa nchini ya Ubelgiji.
Lukaku alifunga mabao mawili kwenye sare ya mabao 3-3 dhidi ya Mexico hivyo kufikisha mabao 30 sawa na Paul Van Himst na Bernard Voorhoof ambao wanashikilia rekodi hiyo.
Lukaku anafanya vizuri msimu huu akiwa na Manchester United ambapo tayari amefunga mabao saba kwenye ligi kuu soka nchini England. Lukaku anaweza kuvunja rekodi siku ya jumanne ambapo Ubelgiji itacheza mechi ya kirafiki na Japan.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni