Rais wa Marekani na Korea Kaskazini wamerejelea vita vyao vya maneno kufuatia mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini.
Wizara ya mashauri ya nchi za kigeni wa Korea Kaskazini ilimuita Trump kuwa "mchochezi wa vita na mzee" na kusisitiza kuwa haiwezi kamwe kuachana na mipango yake ya nyuklia.
Rais Trump alijibu kwa kuandika katika mtandao wake wa kijamii wa Tweeter kuwa, anashangaa ni kwa namna gani Kiongozi wa Korea Kaskazini anamuita mzee.
Trump: Ni kitu kimoja tu kitafanya kazi dhidi ya Korea Kaskazini
CIA: Hakuna uwezekano wa kutokea vita vya nuklia na Korea Kaskazini
Korea Kaskazini: CIA wanapanga kumuua Kim Jong-un
Kile unachohitaji kufahamu kuhusu Korea Kaskazini
Kwa maneno yake, Bwana Trump alisema kuwa hatamuita Rais Kim Jong-un, kuwa mtu "mfupi na mnene".
Anasema kuwa anajaribu sana kwamba siku moja atakuwa rafiki wake wa karibu.
Trump awali alimkejeli kiongozi huyo mkuu wa Korea Kaskazini, kwa kumuita mwendawazimu na 'mtu wa kuunda zana za roketi'.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni