Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mambo yako vipi kwa Air Tanzania hii leo?



Air Tanzania: Faida ikoje baada ya kufufuliwa shirika la ndege Tanzania?



Ndege ya Dreamliner ilipowasili Tanzania Julai 2018

Wiki hii shirika la ndege nchini- Air Tanzania linaidhinisha njia mpya ya usafiri - jambo linalotazamwa kuwa fursa ya ukuwaji linapokuja sula la usafiri wa abiria.

Rais John Pombe Magufuli aliahidi kwamba shirika hilo litaimarishwa na ndege mpya kununuliwa mara baada ya kuingia madarakani.

Tanzania, kama ilivyo kwa nchi nyingine kama Zambia, Zimbabwe, Nigeria na Uganda, imelifufua shirika lake la ndege, ama kama lijulikanavyo, Air Tanzania.


Uwekezaji mkubwa umefanywa mpaka sasa katika kulifanikisha hilo.

"Shirika letu la ndege lilikuwa na hali mbaya sana, lilikuwa na ndege moja tu tena ilikuwa inafanyiwa matengenezo mara kwa mara, soko la ATCL lilishuka sana hadi kufikia asilimia 2.5.

Lakini sasa tumenunua ndege 7, na nyingine kubwa aina ya Boeing 787-8 Dreamliner itakuja mwaka 2020", alisema Rais Magufuli mwaka jana 2018 katika hafla ya kuipokea ndege mpya ya Tanzania.


Rais Magufuli akiwa ndani ya Air Tanzania mnamo 2018

Mambo yako vipi kwa Air Tanzania hii leo?

Mkurugenzi mtendaji wa Air Tanzania Ladislaus Matindi anasema shirika la ndege linapanuka, lakini sio hilo tu ila pia linadhihirisha namna shirika hilo lilivyopiga hatua katika suala la hisa katika soko.

Wakati Air Tanzania likianza, Matindi anaeleza kwamba lilikuwa linadhibiti 2% pekee ya hisa hiyo ya soko.

Precision na Fast Jet zikishikilia sehemu kubwa ya soko wakati huo. Kufikia sasa mkurugenzi huyo mtendaji anasema shirika hilo limesogeza udhibiti kwa zaidi ya 75%.

Akizungumza na BBC, Matindi ameeleza kwamba ufanisi huo umetokana na namna washindani wao walivyokuwa wakihudumu.

Kampuni ya ndege ya Precision ilitumia ndege ndogo na kusafiri katika maeneo machache, Fast jet ambayo haipo sokoni kwa sasa, anasema mbinu waliokuwa wakitumia ya safari za gharama ndogo ni ngumu kuimudu katika mataifa ya Afrika.

Licha ya kwamba ni mbinu inayoonekana kulifaa soko la maeneo masikini, Matindi anafafanua kuwa kiwango cha watu wanaosafiri kutoka maeneo hayo haizidi 2% ya wanaosafiri kwa ndege.

Ili kupata ufanisi wa mbinu hiyo, 'ni lazima uwe na idadi kubwa ya wateja, ili ndege ijaye saa zote, na kuwe na mzunguko mkubwa wa safari hizo' anasema.

Anaeleza kwamba taswira nchini Tanzania ni kwamba idadi kubwa ya watu wako radhi kusafiri safari ndefu kwa basi, kwasababu hawawezi kumudu gharama za tiketi ya ndege.

Hatahivyo anatazama nafasi kwa shirika la ndege la Air Tanzania kutokana na kwamba idadi ya watu walio na kipato cha wastani inaongezeka nchini, na hilo anasema ni fursa kubwa kwa shirika hilo.

Hususan katika msimu kama huu wa sasa kunakoshuhudiwa wasafari wengi, hiyo inamaanisha kwamba shirika linafanikiwa kuuza tiketi za viti vyote katika ndege zinazosafiri za shirika hilo.

Air Tanzania ina ndege ngapi?

Shirika la Air Tanzania lina ndege saba, baada ya kununuliwa ndege sita chini ya mpango wa kufufua shirika hilo lililoanzishwa mwaka 1977.

Kuna Bombardier DASH8 Q400 tatu, mbili ambazo zilifika Tanzania Septemba 2016 na moja Juni 2017; Bombardier CS300 mbili na Boeing 787 Dreamliner ambazo zilitua Tanzania kati ya mei na Julai 2018.

Shirika hilo lilikuwa na Bombardier DASH8 Q300 moja ambayo ilikuwa ikihudumu tangu 2011.

Air Tanzania inamilikiwa asilimia mia moja na serikali kama ilivyo kwa mashirika ya ndege kama Ethiopia.

Kama mashirika mengine ya ndege katika bara la Afrika yalioshindwa kupata ufanisi, Air Tanzania kadhalika iliathirika kutokana baadhi ya mengine, shinikizo la soko.

Afisa mkuu mtendaji wa Air Tanzania anaeleza kuwa kipindi hicho kigumu kilitokana na utovu wa nidhamu ya biashara, akitaja mfano wa wakati ndege ikiwa angani, waziri aliyetarajiwa kuabiri ndege hiyo akachelewa, ndege inalazimishwa kurudi.


Anasema ni jambo lililokuwa likifanyika na sio tu kwa Air Tanzania, kwahivyo anaeleza kwamba kuna suala la ushindani na nidhamu kwa soko.

'Fedha zilizokuwa zikiundwa, zilikuwa ni za watu binafsi katika kampuni hiyo na sio shirika la ndege'.


Matindi anasema wakati wakiidhinisha kufufuliwa kwa ndege hiyo, katika mapato yanayotokana na usafirishaji mizigo, kipato kilikwea kwa kasi kutoka milioni mbili hadi milioni mia mbili kwa mwezi.

Jambo ambalo anasema linadhihirisha kuwa yote ni kutokana na nidhamu ya biashara ambayo haikuwepo katika siku za nyuma.

Ametaja mifano ya mashirika ya ndege yaliojaribu kufufuka kama Air Africa ilivyosambaratika, Air Tanzania ilivyoingia katika matatizo na hata Uganda Air, na kila mtu akiwa anajaribu kufufua mashirika hayo ya ndege pasi kutambua tatizo halisi ni lipi.

Kimsingi Matindi anasema siri ya Air Tanzania sasa, ni kukumbatia nidhamu ya biashara na kutambua kwamba mapato ya fedha ni ya shirika hilo la ndege

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...