Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za Soka Ulaya Jumatatu 1

Tetesi za Soka Ulaya Jumatatu 15.07.2019: Harry Maguire, Lewis Dunk, Kieran Tierney, Leroy Sane


Manchester United inalipa Ā£80m kumsajili Harry Maguire

Manchester United imeafikiana na Leicester makubaliano ya thamani ya Ā£80m kumsajili Harry Maguire na kumfanya kuwa mlinzi mwenye thamani kubwa katika historia.


United italipa Ā£60m kumsajili mchezaji huyo mwenye miaka 26 - atakayefanyiwa ukaguzi wa kiafya leo Jumatatu - na Ā£20m za ziada katika siku zijazo. (Sun)

Leicester inatarajiwa kuijaza nafasi ya Maguire kwa kumsajili mchezaji wa Brighton Lewis Dunk, baada ya kuafikiana kwa mkataba wa thamani ya Ā£45m kwa mchezaji huyo wa miaka 27. (Sun)

Celtic imekataa ombi la Arsenal la hivi karibuni linalokisiwa kuwa na thamani ya Ā£25m - ili kumsajili beki wa kushoto mwenye miaka 22 Kieran Tierney. (Sky Sports)


Manchester City inaamini Leroy Sane ataisusia Bayern Munich iwapo itawasilisha ombi la kumsajili winger huyo wa Ujerumani mwenye miaka 23. (Daily Mirror)

Tottenham na Arsenal zimejiunga na Manchester City katika kumfukuzia beki kamili wa Brazil Dani Alves mwenye umri wa miaka 36, ambaye ni ajenti huru tangu alipoondoka Paris St-Germain. (Mundo Deportivo kupitia Daily Mail)


Tottenham na Arsenal zimejiunga na Manchester City katika kumfukuzia beki kamili wa Brazil Dani Alves

Atletico Madrid haina ushahidi wa kuthibitisha tuhuma kwamba Barcelona ilikuwa na makubaliano tayari na mchezaji wa kiungo cha mbele wa Ufaransa Antoine Griezmann, mwenye umri wa miaka 28, mapema mwezi Machi, kwa mujibu wa rais wa Barca Josep Maria Bartomeu. (Goal)

Mchezaji anayelengwa na Arsenal, Everton mwenye umri wa miaka 23 anayeichezea Gremio, anasema amepewa pendekezo lakini amekataa kufichua jina la klabu iliyomfuata. (Mirror)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp anasema klabu hiyo itaendelea kuweka wazi matumaini yake kuhusu kumsajili beki wa kushoto kuichukua nafasi ya mchezaji wa kimataifa wa Uskotchi Andrew Robertson, mwenye umri wa miaka 25, wakati wa dirisha la uhamisho msimu wa joto. (ESPN)

Aliyekuwa winga wa Newcastle Chris Waddle anaamini kuidhibiti Magpies itakuwa changamoto kubwa katika miaka 21 ya usimamizi wa Steve Bruce iwapo ataondoka Sheffield Jumatano kuelekea St James' Park. (Newcastle Chronicle)

Mchezaji wa kiungo cha kati wa Liverpool Herbie Kane, anatarajiwa kukamilisha uhamisho wa mkopo kwenda katika klabu ya ubingwa wiki hii. Brentford, Charlton na Hull zote zinataka kumsajili mchezaji huyo wa miaka 20 aliyeichezea Doncaster msimu ulioipita. (Goal

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...